Skip to main content

Posts

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA KANDA YA UJENZI YA NYANDA ZA JUU KUSINI

Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) linatarajia kuanzisha  Kikosi  kazi  cha ujenzi wa barabara za lami ,  Ambacho kitafanya kazi sehemu mbali mbali nchini. Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali  Petro Ngata A amezungumza hayo tarehe 02 Agosti 2022, alipofanya ziara katika kanda ya ujenzi ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.

JKT KUENDELEA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO ZA UPATIKANAJI WA MAFUTA YA KULA NCHINI

 Mkurugezi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa( SUMAJKT), Kanali Petro Ngata amesema Jeshi la Kujenga Taifa litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa mafuta ya kula hapa nchini. Ameyasema hayo wakati alipotembelea Banda la JKT katika Maonesho ya Waku- lima,Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) yanayofanyika Kitaifa katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole Jijini Mbeya. Kanali Ngata amefafanua kuwa, JKT limeanza kutekeleza Kilimo cha Mazao ya Kimkakati ikiwemo zao la Alizeti kwa kutumia mashamba yake makubwa katika maeneo ambayo zao hilo linastawi. "Tumeanza na Mkakati wa Kulima kwa wingi mazao ya kimkakati, na hatua inayofuata ni kuchakata zao hilo na kupata mafuta ya Kula". Amesema Kanali Ngata Akizungumzia namna JKT mashamba darasa ya JKT yalivyo na Manufaa, Kanali Ngata amesema JKT lina wataalamu wa kutosha waliobobea katika kutoa elimu bora ya Uzalishaji wa Mazao ya kilimo, Mifugo na Uvuvi hivyo amewataka

ZIARA YA KAMATI YA UTENDAJI SUMAJKT (KUS) KATIKA UJENZI WA MJI WA SERIKALI MTUMBA.

 Mkurugenzi wa fedha wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Luteni Kanali Godfrey Kipingu, ameipongeza Kampuni ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited kwa hatua ya ujenzi wa majengo mbali mbali ya serikali yanayoendelea kujengwa jijini Dodoma. Luteni Kanali Kipingu ametoa pongezi hizo tarehe 01 Agosti 2022, akiwa na Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT (KUS) katika ziara ya Shule ya mfano iliyopo Iyumbu pamoja na majengo nane ya serikali yanayoendelea kujengwa katika mji wa serikali Mtumba Dodoma.

DC MTATIRO AZINDUA SHAMBA LA KOROSHO LA SUMAJKT TUNDUMA

 

KARIBU SUMAJKT LEATHER PRODUCTS KWA BIDHAA HALISI ZA NGOZI

 Kiwanda cha bidhaa za Ngozi SUMAJKT Leadher product kinazalisha bidhaa mbali mbali kwa kutumia ngozi halisi ikiwemo mikoba ya aina mbali mbali, mikanda, viatu vya aina tofauti yani buti kwa ajili ya makampuni ya ulinzi, viatu vya shule, viatu Vya ofisini kwa jinsia zote, tizama video hiyo uweze kuviona . karibu

PONGEZI KWA MKUU WA JKT NA SUMAJKT-DC MTATIRO

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Julius Mtatiro, ameahidi kuongeza mikakati ya uwekezaji katika shamba la kilimo cha korosho na ufugaji wa ng'ombe,  mbuzi na kuku linalomikiwa na Shirika la Uzalishaji  Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) katika Wilaya ya Tunduru. Mhe. Mtatiro, amezungumza hayo leo tarehe 22 Julai 2022, alipokuwa akizindua shamba hilo lililopo katika kijiji cha Nanjoka, Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma. Katika uzinduzi huo Mhe. Julius Mtatiro, ametoa pongezi kwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele na pia kwa Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata kwa kazi kubwa  ambayo wamedhamiria kwenye wilaya ya Tunduru.  "Naishukuru SUMAJKT kwa kulichagua eneo hili kuendesha shughuli za kilimo pamoja ufugaji, ambazo zitakuza uchumi na kuzalisha ajira kwa wingi katika maeneo yetu mbalimbali ", alisema Mhe. Mtatiro.  Mhe. Julius Mtatiro, amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tunduru Bw.

ZINGATIENI UBORA KATIKA MIRADI YA UJENZI-KANALI NGATA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amekagua Miradi tisa ya ujenzi jijini Dodoma inayojengwa na SUMAJKT Construction Company Ltd, kupitia Kanda mbali mbali. Kanali Petro Ngata, amefanya ziara hiyo jana tarehe 22 Julai 2022 alipotembelea  miradi mbali mbali ya ujenzi katika mji wa serikali Mtumba , Shule ya Mfano Iyumbu pamoja ukaguzi wa mitambo katika kiwanda cha mabati SUMAJKT Roofing Company Limited kilichopo Dodoma. Pia amekagua maendeleo ya Ujenzi wa jengo la wizara ya Katiba na Sheria, unaotekelezwa na SUMAJKT Construction Company Limited Ujenzi kanda ya Mashariki,    Pia amekagua Ujenzi wa jengo la Mwanasheria Mkuu wa Serikali unaotekelezwa na  SUMAJKT ujenzi Kanda ya Kati Dodoma, Ujenzi wa Jengo la Wakili Mkuu wa Serikali  unaotekelezwa na SUMAJKT  Makao Makuu, Ujenzi wa Jengo la Wakala wa Mtandao wa Serikali, Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya waziri mkuu, jengo la  Sera,  Ujenzi wa jengo la ofisi ya Waziri Mkuu jen

WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA MWAKA 2022 AWAMU YA PILI

  JESHI la Kujenga Taifa (JKT), tunatoa siku tatu kwa vijana walioitwa kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2022, ambao hawajaripoti mpaka sasa kuripoti makambi waliyopangiwa ya JKT mara moja. Pia tumetoa nyongeza ya majina ya vijana waliohitimu elimu ya kidato cha sita mwaka 2022 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2022. Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali, Hassan Mabena anatoa wito kwa vijana waliochaguliwa wa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria mwaka 2022 Awamu ya Pili ambayo yanatarajiwa kuanza rasmi wiki ijayo na yataendeshwa kwa muda wa miezi mitatu.  Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele anawataka kuripoti makambini vijana wote walioitwa kuhudhuria Mafunzo ya JKT Kwa Mujibu wa Sheria kwa mwaka 2022, ambao hawajaripoti mpaka sasa mripoti makambi ya JKT mara moja. Vijana  waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti makambi ya JKT yaliyo karibu na maeneo wanayoishi. "Vijana wote waliochaguliwa  

SUMAJKT YAKABIDHIWA MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA JAMII YA WAKAZI KUTOKA NGORO NGORO

Taasisi ya Hifadhi ya Ngorongoro ( Ngoro ngoro Conservation Area Authority ( NCAA)  imekabidhi Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga  Taifa ( SUMAJKT) Mradi wa Ujenzi wa nyumba 400 eneo la  Msomela mkoani Tanga kwa  ajili ya Makazi ya jamii ya kimasai kutoka  Ngorongoro mkoani Arusha. Akikabidhiwa Mradi huo tarehe 21 Juni 2022, Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT kanali Petro Ngata amesema kuwa, SUMAJKT ipo tayari kukamilisha kazi hiyo kwa wakati  na kwa ufanisi.                                       "Shirika hili limekuwa likipokea kazi mpya na zilizoshindwa na kampuni nyingine  na kuzikamilisha kwa weledi wa hali ya juu"alisema Kanali Ngata. Nae Mhandisi Joshua Mwankunda kutoka NCAA amesema tayari wamekwisha kamilisha mahitaji muhimu ya awali ikiwemo Michoro, Barabara, Shule, mipaka pamoja na njia za mawasiliano. Mhandisi Joshua ameeleza kuwa tathmini ya mradi huo inaonesha Utagharimu Fedha za Kitanzania Shilingi Bilioni Tisa(9). "Tunaimani kubwa na SUMAJKT kwa ute

KWA MAHITAJI YA OFISI ZA KISASA NA KUMBI KARIBU SUMAJKT HOUSE

SHIRIKA la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) linapangisha  jengo la kisasa ambalo  Limegharimu zaidi ya Bilioni mbili (2) katika kuhakikisha kuwa linafikia viwango vya kisasa. Jengo hilo la kitega uchumi lenye ghorofa tano katika jiji la Dodoma litachangia kasi ya ukuaji wa uchumi nchini. Jengo hilo lijulikanalo kama ‘SUMAJKT HOUSE ’ , lililopo  eneo la Ipagala Mashariki katika kiwanja namba 130 jijini Dodoma, barabara kuu kutoka jijini Dar es Salaam, lina baadhi ya ofisi zitazopangishwa kwa Taasisi mbalimbali ikiwemo Benki, Mashirika na watu binafsi kwa matumizi ya kiofisi. Ghorofa  ya chini na Mezza nine katika jengo hilo itakuwa maalumu kwa ajili ya kupangisha Benki mbalimbali zitakazokuwa na uhitaji, ambapo miundo mbinu yake imejengwa kwa kuzingatia  Ghorofa ya kwanza itatumiwa kwa ofisi za SUMAJKT .  Ghorofa ya pili na ya tatu itakuwa na ofisi zitakazopangwishwa kwa wahitaji. Aidha, ghorofa ya nne itatumika kwa ukumbi kwa matumizi mbalimbali kama mikutano, shereh

WITO WA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT MUJIBU WA SHERIA MWAKA 2022

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linawaita vijana waliohitimu elimu ya Sekondari kidato cha sita kwa mwaka 2022 kutoka shule zote za Tanzania bara kuhudhuria Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria. Sanjari na wito huo, JKT limewapangia makambi watakayokwenda kupatiwa mafunzo na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 03 hadi June 2022. Vijana walioitwa wamepangwa katika kambi za JKT Rwamkoma-Mara, JKT Msange-Tabora, JKT Ruvu-Pwani, JKT Mpwapwa na Makutupora JKT-Dodoma, JKT Mafinga-Iringa, JKT Mlale-Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba-Tanga, JKT Makuyuni-Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa na JKT Mtabila -Kigoma, JKT Itaka-Songwe, JKT Luwa na JKT Milundikwa -Rukwa, JKT Nachingwea-Lindi na JKT Kibiti-Pwani na Oljoro JKT-Arusha. Wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (Physical disabilities) waripoti katika kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia watu wa jamii hiyo. JKT inawataka vijana hao kuripoti wakiwa na vifaa vifuatavyo.     1. Bukta ya

“NAENDELEZA KAZI NINAZOZIJUA”- MEJA JENERALI MABELE

 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT ) Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele tarehe 19/5/2022 ametimiza mwaka Mmoja madarakani huku akiendelea kutekeleza vema  azma ya Jeshi la Kujenga Taifa kujilisha pamoja na malezi ya vijana. Aidha tarehe 19 Mei 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alimteua kwa kipindi hicho akiwa  Brigedia Jenerali Rajabu Nduku Mabele kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afsa mtendaji mkuu wa SUMAJKT  Hatua iliyokuja kufuatia  aliyekuwa Mkuu wa Jeshi hilo, Meja Jenerali Charles Mbuge kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera akichukua nafasi ya Brig Jenerali Marco Elisha Gaguti aliyehamishiwa Mtwara. katika kipindi cha Mwaka mmoja akiwa madarakani Meja Jenerali Mabele ameendelea kutekeleza Majukumu yake kwa weledi ikiwa ni pamoja na kuliongoza vema Jeshi la Kujenga Taifa na Shirika lake la Uzalishaji Mali SUMAJKT. Shirika la Uzali

MWAKA MMOJA WA MKUU WA JKT NA AFISA MTENDAJI MKUU SUMAJKT KATIKA UONGOZI WAKE

KATIKA KUTIMIZA MWAKA MMOJA WA UONGOZI WA MKUU WA JKT NA AFISA MTENDAJI MKUU SUMAJKT HAYA NDIO YALIYOJIRI. SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI   LA KUJENGA TAIFA (SUMAJKT) LINAENDELEA KUPIGA HATUA KATIKA SEKTA YA VIWANDA, SEKTA YA UJENZI, UHANDISI NA USHAURI, SEKTA YA HUDUMA NA BIASHARA, SEKTA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI. KATIKA KIPINDI CHA MWAKA MMOJA WA UONGOZI WA MKUU WA JESHI LA KUJENGA TAIFA NA AFISA MTENDAJI MKUU WA SUMAJKT MEJA JENERALI RAJABU NDUKU MABELE SHIRIKA LIMEPATA MAFANIKIO MBALIMBALI . KWANZA KATIKA SEKTA YA VIWANDA. NOVEMBA 04, 2021 SHIRIKA LILIZINDUA KIWANDA CHA KUTENGENEZA TAA  SUMAJKT SKYZON COMPANY LIMITED SAMBAMBA NA UZINDUZI WA MAGARI NA ZANA NA KILIMO MLALAKUWA JIJINI DAR ES SALAAM. VILE VILE OCTOBA 29, 2021 MEJA JENERALI MABELE ALIZINDUA KIWANDA CHA UTENGENEZAJI MABATI SUMAJKT ROOFING COMPANY LIMITED AMBACHO HIVI SASA TAYARI KIMESIMIKWA MITAMBO JIJINI DODOMA. AIDHA SHIRIKA LIMEPIGA HATUA KATIKA SEKTA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI. PIA KUSIMIKWA MITAMBO YA KUTENGENEZA

KAMPUNI YA USAFI SUMAJKT CLEANING AND FUMIGATION YAPONGEZWA

Video hiyo ni Meneja wa kituo cha mabasi cha Mbezi Luis Bwana Mayira Mkama akipongeza Kampuni ya Usafi SUMAJKT Cleaning and Fumigation kwa huduma nzuri wanayotoa.  Katika mahojiano na SUMAJKT TV tarehe 09 April 2022 Meneja Mayira alisema  kuwa SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co. Limited wanatoa huduma nzuri kituoni hapo kutokana na kuwa na Watendaji wa kutosha pamoja na vitendea kazi vya kutosha tofauti na makampuni mengine ambapo mwanzoni huleta wafanyakazi wengi na baadae hupungua na eneo la kufanya usafi ni kubwa. Aidha ameeleza kuwa Uongozi wa Mbezi Luis Bus Terminal umekuwa ukishirikiana na kampuni hiyo katika kuhakikisha jukumu hilo linatimizwa ipasavyo. Meneja Mayira amezisihi kampuni zingine za usafi kuiga mfano kwa SUMAJKT. SUMAJKT Cleaning and Fumigation Company Limited ni kampuni tanzu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) iliyojizatiti katika utoaji wa huduma ya usafi na unyunyiziaji dawa.  Kampuni imejizatiti katika utoaji wa huduma za usafi kat

HII NDIO SIRI YA MAFANIKIO YA KIWANDA CHA USHONAJI NGUO SUMAJKT GARMENTS COMPANY LIMITED

Katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali kupitia mageuzi ya viwanda Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) halikubaki nyuma katika sekta ya viwanda. Miongoni mwa viwanda vilivyoanzishwa mwaka 2017 SUMAJKT Garments ni kiwanda kimojawapo ambacho kinafanya vizuri katika soko la ushindani na kimekuwa kimbilio la jamii kutokana na umahiri katika kazi ya ushoni. SUMAJKT Garments Company Limited inafanya vizuri katika shughuli za ushonaji nguo na Kupitia Video hiyo utapata kujua shughuli zote za ushonaji nguo sambamba na kudarizi  vinavyofanyika  kiwandani hapo.  Mnamo tarehe 2/02/2022 Kamera za SUMAJKT TV zilifika kiwandani hapo kufuatilia mchakato mzima wa ushonaji nguo na kupitia video hiyo hayo ndio yaliyojiri. Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Sylvester Ntandu pamoja na Maafisa wasaidizi wake wanakuelezea utendaji kazi wa kiwanda hicho. SUMAJKT Garments Company Limited kinashona mavazi ya aina mbali mbali zikiwemo nguo za watu binafsi, sare z