Skip to main content

HII NDIO SIRI YA MAFANIKIO YA KIWANDA CHA USHONAJI NGUO SUMAJKT GARMENTS COMPANY LIMITED




Katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali kupitia mageuzi ya viwanda Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) halikubaki nyuma katika sekta ya viwanda.

Miongoni mwa viwanda vilivyoanzishwa mwaka 2017 SUMAJKT Garments ni kiwanda kimojawapo ambacho kinafanya vizuri katika soko la ushindani na kimekuwa kimbilio la jamii kutokana na umahiri katika kazi ya ushoni.

SUMAJKT Garments Company Limited inafanya vizuri katika shughuli za ushonaji nguo na Kupitia Video hiyo utapata kujua shughuli zote za ushonaji nguo sambamba na kudarizi  vinavyofanyika  kiwandani hapo. 

Mnamo tarehe 2/02/2022 Kamera za SUMAJKT TV zilifika kiwandani hapo kufuatilia mchakato mzima wa ushonaji nguo na kupitia video hiyo hayo ndio yaliyojiri.

Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Sylvester Ntandu pamoja na Maafisa wasaidizi wake wanakuelezea utendaji kazi wa kiwanda hicho.

SUMAJKT Garments Company Limited kinashona mavazi ya aina mbali mbali zikiwemo nguo za watu binafsi, sare za vyombo vya ulinzi na usalama, sare za shule, sare za makampuni na taasisi mbali mbali. 

Pia kiwanda kinadarizi nembo za aina mbali mbali pamoja na kuchapa nguo.

Aidha, Kiwanda hicho kimekuwa kikiunga mkono juhudi za serikali kwa kutoa ajira kwa vijana sambamba na fursa ya kujifunza kwa vitendo bure .
 
Kiwanda kipo Mgulani JKT Dar es Salaam, kwa mawasiliano zaidi piga 
Simu namba +255 718 488 234 au 
Barua Pepe: info@sumajkt.go.tz





















Comments

Popular posts from this blog

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.