Katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali kupitia mageuzi ya viwanda Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) halikubaki nyuma katika sekta ya viwanda.
Miongoni mwa viwanda vilivyoanzishwa mwaka 2017 SUMAJKT Garments ni kiwanda kimojawapo ambacho kinafanya vizuri katika soko la ushindani na kimekuwa kimbilio la jamii kutokana na umahiri katika kazi ya ushoni.
SUMAJKT Garments Company Limited inafanya vizuri katika shughuli za ushonaji nguo na Kupitia Video hiyo utapata kujua shughuli zote za ushonaji nguo sambamba na kudarizi vinavyofanyika kiwandani hapo.
Mnamo tarehe 2/02/2022 Kamera za SUMAJKT TV zilifika kiwandani hapo kufuatilia mchakato mzima wa ushonaji nguo na kupitia video hiyo hayo ndio yaliyojiri.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Sylvester Ntandu pamoja na Maafisa wasaidizi wake wanakuelezea utendaji kazi wa kiwanda hicho.
SUMAJKT Garments Company Limited kinashona mavazi ya aina mbali mbali zikiwemo nguo za watu binafsi, sare za vyombo vya ulinzi na usalama, sare za shule, sare za makampuni na taasisi mbali mbali.
Pia kiwanda kinadarizi nembo za aina mbali mbali pamoja na kuchapa nguo.
Aidha, Kiwanda hicho kimekuwa kikiunga mkono juhudi za serikali kwa kutoa ajira kwa vijana sambamba na fursa ya kujifunza kwa vitendo bure .
Kiwanda kipo Mgulani JKT Dar es Salaam, kwa mawasiliano zaidi piga
Simu namba +255 718 488 234 au
Barua Pepe: info@sumajkt.go.tz
Comments
Post a Comment