Aidha tarehe 19 Mei 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alimteua kwa kipindi hicho akiwa Brigedia Jenerali Rajabu Nduku Mabele kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afsa mtendaji mkuu wa SUMAJKT Hatua iliyokuja kufuatia aliyekuwa Mkuu wa Jeshi hilo, Meja Jenerali Charles Mbuge kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera akichukua nafasi ya Brig Jenerali Marco Elisha Gaguti aliyehamishiwa Mtwara.
katika kipindi cha Mwaka mmoja akiwa madarakani Meja Jenerali Mabele ameendelea kutekeleza Majukumu yake kwa weledi ikiwa ni pamoja na kuliongoza vema Jeshi la Kujenga Taifa na Shirika lake la Uzalishaji Mali SUMAJKT.
Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa(SUMAJKT) linaendelea kupiga hatua katika sekta ya viwanda, sekta ya ujenzi, uhandisi na ushauri, sekta ya huduma na biashara, sekta kilimo, mifugo na uvuvi.
katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele Shirika limepata mafanikio mbalimbali .
Tukianza na sekta ya viwanda, Novemba 04, 2021 Shirika lilizindua kiwanda cha kutengeneza taa SUMAJKT Skyzon Company Limited sambamba na uzinduzi wa magari na zana na kilimo Mlalakuwa jijini Dar es salaam.
Vile vile octoba 29, 2021 Meja Jenerali Mabele alizindua kiwanda cha utengenezaji mabati SUMAJKT Roofing Company Limited ambacho hivi sasa tayari kimesimikwa mitambo jijini Dodoma.
Aidha Shirika limepiga hatua katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.
Pia kusimikwa mitambo ya kutengeneza viatu katika kampuni ya viatu SUMAJKT Leather Product Company Limited.
Ukamilishwaji wa jengo la biashara la SUMAJKT Tower jijini Dodoma.
Shirika linaendelea kukua kwa kasi na hayo ni baadhi tu ya mafanikio . Kasi hii ya ukuaji wa Shirika la JKT ni faida kwa taifa na kwa vijana ambao ndio taifa la kesho na juhudi hizi zinastahili pongezi.
Meja Jenerali Mabele alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tarehe 25 Novemba 1993 na kutunukiwa Kamisheni kuwa Afisa tarehe 25 Machi 1995. Pamoja na taaluma nyingine za Kijeshi, Jenerali Mabele ana Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Biashara (Master of Business Administration), akijikita katika Usimamizi wa Mashirika yaani (Corporate Management).
Katika utumishi wake Meja Jenerali Mabele amewahi kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo Afisa Usalama na Utambuzi katika Vikosi kadhaa, Afisa Mnadhimu Malipo na Afisa Malipo wa Kikosi Makao Makuu ya Jeshi, Mkurugenzi wa Fedha za Umma na Uhasibu (Director for Public Finance and Accounting) na baadae alihamishiwa Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), nafasi aliyohudumu hadi kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.
Hongera sana kwa kutimiza mwaka mmoja madarakani ambapo mafanikio hayo yaliyotajwa kwa uchache yamechangiwa na juhudi zako za kujituma, uchapakazi, matumizi mazuri ya fedha, weledi, usimamizi bora wa rasilimali watu chini yako tunajivunia mchango wako katika Jeshi la Kujenga Taifa. Asante
Comments
Post a Comment