JESHI la Kujenga Taifa (JKT), tunatoa siku tatu kwa vijana walioitwa kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2022, ambao hawajaripoti mpaka sasa kuripoti makambi waliyopangiwa ya JKT mara moja.
Pia tumetoa nyongeza ya majina ya vijana waliohitimu elimu ya kidato cha sita mwaka 2022 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2022.
Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali, Hassan Mabena anatoa wito kwa vijana waliochaguliwa wa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria mwaka 2022 Awamu ya Pili ambayo yanatarajiwa kuanza rasmi wiki ijayo na yataendeshwa kwa muda wa miezi mitatu.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele anawataka kuripoti makambini vijana wote walioitwa kuhudhuria Mafunzo ya JKT Kwa Mujibu wa Sheria kwa mwaka 2022, ambao hawajaripoti mpaka sasa mripoti makambi ya JKT mara moja.
Vijana waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti makambi ya JKT yaliyo karibu na maeneo wanayoishi.
"Vijana wote waliochaguliwa waripoti makambi ya JKT yaliyo karibu na maeneo wanayoishi, isipokuwa Kambi ya Makutupora JKT iliyopo mkoani Dodoma, Chuo Cha Ungozi Cha Jeshi la Kutenga Taifa(CUJKT) iliyopo Kimbiji mkaoni Dar es Salaam na Ruvu JKT iliyopo Mlandizi mkoani Pwani, ambayo inapokea wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho yenye miundombinu ya kuwahudumia watu wa jamii hiyo,"Brigedia Jenerali Mabena.
Vijana wote wanatakiwa kuripoti makambi ya JKT kuanzia tarehe 23 hadi Juni 25 mwaka huu 2022.
Comments
Post a Comment