Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2022

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMEAGA KAYA ZINGINE 25 NGORO NGORO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameaga kaya zingine 25, zenye watu 105, na amesema mpaka kufikia tarehe 18/8/2022,  jumla ya kaya 1,002 zenye watu 5,382 zimejiandikisha kwa hiari kuhama katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro na kuelekea kijiji cha Msomera wilayani Handeni mkoa wa Tanga,  lililotengwa na serikali kwa ajili ya wakazi hao. Kati ya kaya hizo,  tayari kaya 624 zenye watu 3,323 zimehakikiwa na kufanyiwa uthamini na kati ya kaya hizo, kaya 106 zenye watu 536 zimeshahamia kijiji cha Msomera wilayani Handeni Mkoani Tanga. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema hayo Agosti 19,2022 Mkoani Arusha sambamba na zoezi la kukabidhi hundi ya Malipo kwa wakazi wapya wa Msomera. Hafla fupi ilifanyika kwenye ofisi za mamlaka ya hifadhi  hiyo kwa nia ya kufanikisha hatua hiyo. Aidha , Mhe. Kassim Majaliwa ameeleza kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan amepongeza uamuzi wa wananchi hao na kwamba serikali itaendelea kuwekeza katika kuboresha miundombinu ya eneo la Msomera.  “Napenda kumhakikishia Mheshimiwa

FANYIENI UTAFITI MAZAO YA NGANO NA ALIZETI - KANALI NGATA

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo kwa Meneja wa shamba la SUMAJKT Bassotu Sajinitaji Bahati Kidenya, kufanya utafiti mzuri wa mazao ya ngano na alizeti ili shirika likiamua kuwekeza katika kilimo hicho kiwe na tija. Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo  hayo leo tarehe  12 Augosti 2022, alipokuwa katika ziara ya kukagua shamba hilo lililopo katika kijiji cha Bassotu , Wilaya ya Hanang'i Mkoani Manyara.  Kanali Ngata ameongeza kuwa  Bassotu kuna faida kubwa endapo SUMAJKT itafanikiwa kupata eneo kubwa na kuanza na aina ya mazao mawili ambayo ni ngano na katamu (alizeti za miba). "Ngano na katamu ni mazao ambayo tukizalisha tutakuwa na uhakika wa kupata faida" ameeleza Kanali Ngata.  Aidha, Kanali Petro Ngata,  ameeleza kuwa shirika litaanza kuliwekea mipango mizuri na ya haraka shamba hilo, endapo msajili wa hazina atakubali kutoa eneo kwa SUMAJKT.      Kwa upande wa Meneja wa mradi wa sh

IJUE SIRI YA MAFANIKIO YA JKT KATIKA KILIMO

MKUU wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema pamoja na kuwa na mabadiliko ya tabia nchi lakini bado katika vipando vya Jeshi la kujenga taifa na mashamba yake kwa  na vikosi yameendelea kufanya vizuri na mazao yanastawi kwa jinsi ambavyo walikuwa wametalajia. Amesema kuwa wao walishaona changamoto hizo za mabadiliko  ya tabia nchi hivyo walishaanza kufanya mawasiliano na mamlaka ya hali ya hewa ambapo walikuwa wanapewa taarifa juu ya mabadiliko hayo hususani kwenye eneo la mvua kwamba msimu huo mvua zitawahi ama kuchelewa na kama zitawahi zitakuja kwa viwango vidogo. Amesema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo wao kama Jeshi la kujenga taifa walikaa chinin nakuweza kujipanga na kuona aina ya mbegu ambazo zitaweza kuendana na hali ya hewa. Brigedia Mabena ameyasema hayo Agosti 7 kwenye maonyesho ya nanenane ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Mbeya wakati alipotembelea banda la JKT pamoja na mambo mengine amesema kuwa katika kikosi cha 847 KJ ni Milundikwa nakwamba pa

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA KANDA YA UJENZI YA NYANDA ZA JUU KUSINI

Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) linatarajia kuanzisha  Kikosi  kazi  cha ujenzi wa barabara za lami ,  Ambacho kitafanya kazi sehemu mbali mbali nchini. Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali  Petro Ngata A amezungumza hayo tarehe 02 Agosti 2022, alipofanya ziara katika kanda ya ujenzi ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.

JKT KUENDELEA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO ZA UPATIKANAJI WA MAFUTA YA KULA NCHINI

 Mkurugezi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa( SUMAJKT), Kanali Petro Ngata amesema Jeshi la Kujenga Taifa litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa mafuta ya kula hapa nchini. Ameyasema hayo wakati alipotembelea Banda la JKT katika Maonesho ya Waku- lima,Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) yanayofanyika Kitaifa katika viwanja vya John Mwakangale, Uyole Jijini Mbeya. Kanali Ngata amefafanua kuwa, JKT limeanza kutekeleza Kilimo cha Mazao ya Kimkakati ikiwemo zao la Alizeti kwa kutumia mashamba yake makubwa katika maeneo ambayo zao hilo linastawi. "Tumeanza na Mkakati wa Kulima kwa wingi mazao ya kimkakati, na hatua inayofuata ni kuchakata zao hilo na kupata mafuta ya Kula". Amesema Kanali Ngata Akizungumzia namna JKT mashamba darasa ya JKT yalivyo na Manufaa, Kanali Ngata amesema JKT lina wataalamu wa kutosha waliobobea katika kutoa elimu bora ya Uzalishaji wa Mazao ya kilimo, Mifugo na Uvuvi hivyo amewataka

ZIARA YA KAMATI YA UTENDAJI SUMAJKT (KUS) KATIKA UJENZI WA MJI WA SERIKALI MTUMBA.

 Mkurugenzi wa fedha wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Luteni Kanali Godfrey Kipingu, ameipongeza Kampuni ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited kwa hatua ya ujenzi wa majengo mbali mbali ya serikali yanayoendelea kujengwa jijini Dodoma. Luteni Kanali Kipingu ametoa pongezi hizo tarehe 01 Agosti 2022, akiwa na Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT (KUS) katika ziara ya Shule ya mfano iliyopo Iyumbu pamoja na majengo nane ya serikali yanayoendelea kujengwa katika mji wa serikali Mtumba Dodoma.