SHIRIKA la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) linapangisha jengo la kisasa ambalo Limegharimu zaidi ya Bilioni mbili (2) katika kuhakikisha kuwa linafikia viwango vya kisasa. Jengo hilo la kitega uchumi lenye ghorofa tano katika jiji la Dodoma litachangia kasi ya ukuaji wa uchumi nchini. Jengo hilo lijulikanalo kama ‘SUMAJKT HOUSE ’ , lililopo eneo la Ipagala Mashariki katika kiwanja namba 130 jijini Dodoma, barabara kuu kutoka jijini Dar es Salaam, lina baadhi ya ofisi zitazopangishwa kwa Taasisi mbalimbali ikiwemo Benki, Mashirika na watu binafsi kwa matumizi ya kiofisi. Ghorofa ya chini na Mezza nine katika jengo hilo itakuwa maalumu kwa ajili ya kupangisha Benki mbalimbali zitakazokuwa na uhitaji, ambapo miundo mbinu yake imejengwa kwa kuzingatia Ghorofa ya kwanza itatumiwa kwa ofisi za SUMAJKT . Ghorofa ya pili na ya tatu itakuwa na ofisi zitakazopangwishwa kwa wahitaji. Aidha, ghorofa ya nne itatumika kwa ukumbi kwa matumizi mbalimbali kama mikutano, shereh