Skip to main content

Posts

Showing posts with the label Ziara za wageni mbali mbali

UJUMBE WA MAAFISA KUTOKA NCHINI ZAMBIA WATEMBELEA SUMAJKT

Ujumbe wa Maafisa kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu nchini Zambia ukiongozwa na Brigedia Jenerali Humphery Nyone leo tarehe 03 Oktoba 2022 umetembelea Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Makao Makuu Mlalakuwa jijini Dar es salaam ili kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT. Ujumbe huo idadi ya Maafisa 20 umepokelewa na Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Shija Lupi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Elikana Ngata. Akizungumza mara baada ya kupokea Ugeni huo Kanali Shija Lupi amesema kuwa Zambia na Tanzania zimeendeleza Udugu katika Shughuli mbalimbali za Kibiashara. "nchi hizi mbili zimekua kiuchumi,  mara baada ya kupata uhuru katika miaka ya 1960,  na Zambia  kwa mara kadhaa imekua ikiagiza bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania,  ikiwemo vifaa vya ujenzi pamoja na mazao ya vyakula,  lakini pia Zambia imekua mzalishaji mkubwa wa bidhaa za kilimo,  kama mahindi,  bidhaa za shaba na nyingine nyingi" Ai

KAMANDA JKT ZAMBIA ATEMBELEA VIWANDA SUMAJKT

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Tanzania Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele apongezwa na Mkuu wa JKT Zambia kwa kupiga hatua katika kusimamia  uzalishajimali . Kamanda wa Jeshi la Kujenga Taifa Zambia Luteni Jenerali Maliti Solochi tarehe 15 Machi 2022 ametembelea Kiwanda cha maji SUMAJKT Bottling Company pamoja na kiwanda cha ushonaji nguo SUMAJKT Garments Company katika eneo la Mgulani JKT Dar es Salaam kuona uzalishajimali na ametoa pongezi kwa namna Shirika linavyoendeshwa na kupiga hatua chini ya Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajab Nduku Mabele. Jenerali Solochi amesema kuwa JKT Zambia limekopi kila kitu kutoka JKT Tanzania ikiwemo uanzishaji wa viwanda na kwasasa jeshi lao lina baadhi ya viwanda ikiwemo kiwanda cha maji na kiwanda cha viatu. Jenerali Solochi ameongeza kuwa mahusiano haya ya kindugu kati ya JKT Tanzania na JKT Zambia yalianzishwa na Viongozi waasisi wake ambao ni baba wa taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Keneth Kau