Sanjari na wito huo, JKT limewapangia makambi watakayokwenda kupatiwa mafunzo na wanatakiwa kuripoti makambini kuanzia tarehe 03 hadi June 2022.
Vijana walioitwa wamepangwa katika kambi za JKT Rwamkoma-Mara, JKT Msange-Tabora, JKT Ruvu-Pwani, JKT Mpwapwa na Makutupora JKT-Dodoma, JKT Mafinga-Iringa, JKT Mlale-Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba-Tanga, JKT Makuyuni-Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa na JKT Mtabila -Kigoma, JKT Itaka-Songwe, JKT Luwa na JKT Milundikwa -Rukwa, JKT Nachingwea-Lindi na JKT Kibiti-Pwani na Oljoro JKT-Arusha.
Wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (Physical disabilities) waripoti katika kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia watu wa jamii hiyo.
JKT inawataka vijana hao kuripoti wakiwa na vifaa vifuatavyo.
1. Bukta ya rangi ya ‘Dark Blue’ yenye mpira kiunoni (lastic) iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini, isiyo na zipu.
2. T-shirt ya rangi ya kijani
(Green Vest)
3. Raba za michezo zenye
rangi ya kijani au blue.
4. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari.
5. Soksi ndefu za rangi nyeusi.
6. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangiwa mikoa yenye baridi.
7. Track suit ya rangi ya kijani au blue.
8. Nyaraka zote zinazohitajika katika udahili wa kujiunga na elimu ya Juu, zikiwemo cheti cha kuzaliwa, vyeti vya kuhitimu kidato cha Nne n.k
Nauli ya kwenda makambini na kurudi nyumbani.
Orodha kamili ya majina ya vijana walioitwa, Makambi ya JKT waliyopangiwa na maeneo yaliyopo pamoja na vifaa wanavyotakiwa kwenda navyo inapatikana katika tovuti ya JKT ambayo ni www.jkt.go.tz
Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele anawakaribisha vijana wote walioitwa ili waweze kujiunga na vijana wenzao katika kujifunza Uzalendo, Umoja wa kitaifa, Stadi za kazi , Stadi za Maisha na Utayari wa Kulijenga na Kulitumikia Taifa.
Comments
Post a Comment