Taasisi ya Hifadhi ya Ngorongoro ( Ngoro ngoro Conservation Area Authority ( NCAA) imekabidhi Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa ( SUMAJKT) Mradi wa Ujenzi wa nyumba 400 eneo la Msomela mkoani Tanga kwa ajili ya Makazi ya jamii ya kimasai kutoka Ngorongoro mkoani Arusha.
Akikabidhiwa Mradi huo tarehe 21 Juni 2022, Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT kanali Petro Ngata amesema kuwa, SUMAJKT ipo tayari kukamilisha kazi hiyo kwa wakati na kwa ufanisi.
Nae Mhandisi Joshua Mwankunda kutoka NCAA amesema tayari wamekwisha kamilisha mahitaji muhimu ya awali ikiwemo Michoro, Barabara, Shule, mipaka pamoja na njia za mawasiliano.
Mhandisi Joshua ameeleza kuwa tathmini ya mradi huo inaonesha Utagharimu Fedha za Kitanzania Shilingi Bilioni Tisa(9).
"Tunaimani kubwa na SUMAJKT kwa utendaji wao watafanya kile kilichokusudiwa kwa umaridadi mkubwa".Alisema Mhandisi joshua.
Serikali imeihamisha jamii ya Kimasai iliyokuwa ikiishi Ngorongoro mkoani Arusha na kuihamishia eneo la Msomela Tanga ili kuachia eneo la Ngorongoro shughuli za hifadhi ya Taifa ziendelee .
Mradi wa Ujenzi wa nyumba 400 Kwa Makazi ya jamii ya Kimasai kutoka Ngorongoro unapangwa Kutekelezwa Kwa muda wa siku 90.
Comments
Post a Comment