Skip to main content

Posts

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup
Recent posts

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalisahaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo ya kukamilishwa kwa wakati miradi ya ujenzi inayojengwa na Mkandarasi SUMAJKT Construction Co. Ltd Kanda ya Ziwa.  Kanali Petro Ngata akiendelea na ziara katika miradi ya ujenzi kanda ya ziwa, ametembelea  Ujenzi wa majengo ya OPD, RCH, Pharmacy na Mortuary yaliyopo katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza.  Aidha Kanali Ngata ameagiza kasi ya ujenzi iongezwe na ifanyike kwa njia ya oparesheni ambapo majengo ya "Pharmacy" na "Mortuary" yawe yamekamilika ifikapo tarehe 30 Nov 22 na "OPD" na "RCH" yakamilike ifikapo tarehe 12 Dec 22.  Vile vile Kanali Ngata amepata wasaa wa kutembelea Jengo la Halmashauri ya Bunda na kuagiza Meneja Ujenzi Kanda ya Ziwa kumuandikia Mshauri wa Mradi changamoto zote zinazosababisha ucheleweshaji wa mradi huu unaotekelezwa kwa njia ya "Force Account" ili uweze kukamilika kwa w

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata ameendelea na ziara katika miradi mbali mbali ya ujenzi inayoendelea kujengwa na Kampuni ya ujenzi “SUMAJKT Construction Company Limited kupitia SUMAJKT Ujenzi kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata katika ziara hiyo iliyoanza tarehe 28 hadi 30 Oktoba 2022 amekagua miradi mingine  inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa Ujenzi wa hanga la Askari, Jengo la kuhifadhia maiti "Mortuary" na Jengo la wodi ya Wagonjwa Maalumu "VIP Ward" katika Hospitali ya Kijeshi Ilemela- Mwanza,   ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Kanda ya Ziwa lililopo Busweli-Ilemela Jijini Mwanza na kuagiza SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa iongeze kasi ya ujenzi ili ikamilishe mradi huo kwa wakati. Aidha Kanali Petro Ngata amepongeza maendeleo ya utekelezaji wa Miradi hiyo na kuagiza SUMAJKT Ujenzi Kanda ya ziwa kukamilisha Ujenzi wa hanga  la Askari pamoja na c

MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA) KUTOA MILIONI ISHIRINI NA TISA KUKARABATI MADARASA JITEGEMEE SEKONDARI

Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Alphayo Kidato ameahidi kutoa kiasi cha milioni ishirini na tisa za kitanzania kwa ajili yakukarabati Madarasa pamoja na Mabweni ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT iliyopo Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam. Ahadi hiyo imetolewa leo tarehe 29 Octoba 2022 na Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Richard Kayombo kwa niaba ya Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Alphayo Kidato aliyemwakilisha katika mahafali hayo ya 38 ya kidato cha nne 2022. Kayombo alitoa shukrani za pongezi kwa uongozi wa shule ya Jitegemee kwa kuona umuhimu wa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa sehemu ya familia ya Jitegemee katika mahafali ya 38 ya wanafunzi wa kidato cha nne. Pia Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Richard Kayombo amewasihi wahitimu na wanafunzi wengine kuhakikisha wanaongeza nidhamu katika masomo ili w

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MHESHIMIWA BASHUNGWA ALIPONGEZA JKT

  Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Innocent Bashungwa amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kwa kuendelea kutekeleza jukumu la malezi ya Vijana kupitia mafunzo yao ya Kujitolea na Mujibu wa Sheria yanayotolewa kwenye makambi ya JKT ili kuwajengea uzalendo pamoja na stadi za kazi na waweze kushiriki ujenzi wa Taifa. Mhe. Bashungwa amesema hayo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kujitambulisha, Makao Mkuu ya JKT Chamwino, Jijini Dodoma ambapo alipata fursa ya kuongea na Maafisa, Askari, Vijana na Watumishi wa Umma wanaofanyia kazi JKT eneo la Dodoma. Mhe. Bashungwa ameongeza kuwa, Kukamilika kwa miradi ya Kilimo cha kimkakati katika shamba la SUMAJKT lililopo Mngeta na Ujenzi wa miundombinu ya Skimu ya Umwagiliaji iliyopo katika kikosi cha Chita JKT mkoani Morogoro, Italeta tija katika upatikanaji wa chakula cha kutosha na kulihakikishia Taifa Usalama wa Chakula pamoja na upatikanaji wa Mbegu bora. Ameongeza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita imetenga bajeti ya fedha kupitia Wizara ya U

MAISHA NI MAPAMBANO - Meja Misigaro

  NAIBU Kamanda Kikosi cha Mgulani JKT, Meja Eusebius Misigaro amewakumbusha Wanafunzi wahitimu wa mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo katika shule ya Sekondari ya Jitegemee kuwa Maisha ni mapambano ambayo yanahitaji maandalizi mazuri na njia sahihi ya kujiandaa kupata Elimu, maarifa, fikra na ujuzi sahihi. Meja Misigaro ameyasema hayo leo tarehe 21 Oktoba 2022 alipokuwa akifunga mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo kwa Wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka 2022/2023 na wahamiaji wa kidato cha kwanza na kidato cha tatu. Mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo wanayopatiwa wanafunzi wanaoanza Shule katika shule ya Sekondari Jitegemee yana dhima Kuu ambayo ni kumjenga Mwanafunzi na kimaadili ili elimu anayopata iweze kumsaidia kikamilifu katika kupambana na changamoto mbalimbali za maisha ya kila siku sambamba na mwanafunzi kuwa na nidhamu na maadili mema, kwani nidhamu ni msingi wa mafanikio katika maisha.  Elimu ya darasani ni vema iende sambamba na kupandikiza chembechembe za nidhamu Kwa mwanafunz

MHE. RAIS SAMIA SULUHU AMPONGEZA MKUU WA JKT

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan amempongeza Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa kukamilisha ujenzi wa Mradi wa Chuo cha Ualimu Kabanga .  Mhe. Rais Samia Suluhu amesema hayo tarehe 17 Oktoba 2022 katika ufunguzi wa majengo ya chuo hicho kilichopo katika wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma alipokuwa akizindua Mradi huo Aidha mradi huo uliofadhiliwa na Serikali ya Canada Ulianza tarehe 26 Machi 2019 ambapo ulitekelezwa na Kampuni ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited na kukabidhiwa rasmi kwa Wizara ya Elimu baada ya kukamilika tarehe 21 Apri 2022 kupitia Kanda ya ujenzi ya Kusini inayosimamiwa na Kanali Mbaraka Magogo ambaye ni Mkuu wa Ujenzi Kanda ya Magharibi. Thamani ya mradi huo ni TShs 12.1 billion zikiwa ni gharama za mkandarasi na una jumla ya majengo 13 ambayo ni mabweni 2, jengo la utawala, jengo la madaras

UHURU PEAK PURE DRINKING WATER

 

UJUMBE WA MAAFISA KUTOKA NCHINI ZAMBIA WATEMBELEA SUMAJKT

Ujumbe wa Maafisa kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu nchini Zambia ukiongozwa na Brigedia Jenerali Humphery Nyone leo tarehe 03 Oktoba 2022 umetembelea Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Makao Makuu Mlalakuwa jijini Dar es salaam ili kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT. Ujumbe huo idadi ya Maafisa 20 umepokelewa na Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Shija Lupi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Elikana Ngata. Akizungumza mara baada ya kupokea Ugeni huo Kanali Shija Lupi amesema kuwa Zambia na Tanzania zimeendeleza Udugu katika Shughuli mbalimbali za Kibiashara. "nchi hizi mbili zimekua kiuchumi,  mara baada ya kupata uhuru katika miaka ya 1960,  na Zambia  kwa mara kadhaa imekua ikiagiza bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania,  ikiwemo vifaa vya ujenzi pamoja na mazao ya vyakula,  lakini pia Zambia imekua mzalishaji mkubwa wa bidhaa za kilimo,  kama mahindi,  bidhaa za shaba na nyingine nyingi" Ai

MRADI WA UJENZI MTUMBA KUKAMILIKA KWA WAKATI-KANALI PETRO NGATA

Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata amesema mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba unaotekelezwa na kampuni  tanzu ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited (SCCL) utakamilika kwa wakati uliopangwa. Kanali Petro Ngata amesema hayo jana (Jumatatu, Septemba 5, 2022) wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika kukagua maendeleo ujenzi wa Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.  "Mheshimiwa Waziri Mkuu ameridhishwa sana na kazi tunazozifanya hapa katika mji wa serikali Sisi  SUMAJKT tunatekeleza miradi idadi tisa kwa maana ya majengo ya wizara na yote yapo katika hatua nzuri na tunakwenda na wakati kulingana na mkataba ulivyo.  Na sisi kama SUMAJKT kwa kuzingatia maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri Mkuu siku hii ya leo tumejipanga kuhakikisha kwamba tunakamilisha hili jukumu katika muda aliopanga Mheshimiwa Waziri Mkuu."alisema Kanali Ngata.   Nae Meneja wa Ujenzi SUMAJKT-Kanda ya Magharibi Kanali Mbaraka Magogo amesema kuwa mr

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMEAGA KAYA ZINGINE 25 NGORO NGORO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameaga kaya zingine 25, zenye watu 105, na amesema mpaka kufikia tarehe 18/8/2022,  jumla ya kaya 1,002 zenye watu 5,382 zimejiandikisha kwa hiari kuhama katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro na kuelekea kijiji cha Msomera wilayani Handeni mkoa wa Tanga,  lililotengwa na serikali kwa ajili ya wakazi hao. Kati ya kaya hizo,  tayari kaya 624 zenye watu 3,323 zimehakikiwa na kufanyiwa uthamini na kati ya kaya hizo, kaya 106 zenye watu 536 zimeshahamia kijiji cha Msomera wilayani Handeni Mkoani Tanga. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema hayo Agosti 19,2022 Mkoani Arusha sambamba na zoezi la kukabidhi hundi ya Malipo kwa wakazi wapya wa Msomera. Hafla fupi ilifanyika kwenye ofisi za mamlaka ya hifadhi  hiyo kwa nia ya kufanikisha hatua hiyo. Aidha , Mhe. Kassim Majaliwa ameeleza kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan amepongeza uamuzi wa wananchi hao na kwamba serikali itaendelea kuwekeza katika kuboresha miundombinu ya eneo la Msomera.  “Napenda kumhakikishia Mheshimiwa

FANYIENI UTAFITI MAZAO YA NGANO NA ALIZETI - KANALI NGATA

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo kwa Meneja wa shamba la SUMAJKT Bassotu Sajinitaji Bahati Kidenya, kufanya utafiti mzuri wa mazao ya ngano na alizeti ili shirika likiamua kuwekeza katika kilimo hicho kiwe na tija. Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo  hayo leo tarehe  12 Augosti 2022, alipokuwa katika ziara ya kukagua shamba hilo lililopo katika kijiji cha Bassotu , Wilaya ya Hanang'i Mkoani Manyara.  Kanali Ngata ameongeza kuwa  Bassotu kuna faida kubwa endapo SUMAJKT itafanikiwa kupata eneo kubwa na kuanza na aina ya mazao mawili ambayo ni ngano na katamu (alizeti za miba). "Ngano na katamu ni mazao ambayo tukizalisha tutakuwa na uhakika wa kupata faida" ameeleza Kanali Ngata.  Aidha, Kanali Petro Ngata,  ameeleza kuwa shirika litaanza kuliwekea mipango mizuri na ya haraka shamba hilo, endapo msajili wa hazina atakubali kutoa eneo kwa SUMAJKT.      Kwa upande wa Meneja wa mradi wa sh

IJUE SIRI YA MAFANIKIO YA JKT KATIKA KILIMO

MKUU wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema pamoja na kuwa na mabadiliko ya tabia nchi lakini bado katika vipando vya Jeshi la kujenga taifa na mashamba yake kwa  na vikosi yameendelea kufanya vizuri na mazao yanastawi kwa jinsi ambavyo walikuwa wametalajia. Amesema kuwa wao walishaona changamoto hizo za mabadiliko  ya tabia nchi hivyo walishaanza kufanya mawasiliano na mamlaka ya hali ya hewa ambapo walikuwa wanapewa taarifa juu ya mabadiliko hayo hususani kwenye eneo la mvua kwamba msimu huo mvua zitawahi ama kuchelewa na kama zitawahi zitakuja kwa viwango vidogo. Amesema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo wao kama Jeshi la kujenga taifa walikaa chinin nakuweza kujipanga na kuona aina ya mbegu ambazo zitaweza kuendana na hali ya hewa. Brigedia Mabena ameyasema hayo Agosti 7 kwenye maonyesho ya nanenane ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Mbeya wakati alipotembelea banda la JKT pamoja na mambo mengine amesema kuwa katika kikosi cha 847 KJ ni Milundikwa nakwamba pa

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.