Skip to main content

KAMPUNI YA USAFI SUMAJKT CLEANING AND FUMIGATION YAPONGEZWA




Video hiyo ni Meneja wa kituo cha mabasi cha Mbezi Luis Bwana Mayira Mkama akipongeza Kampuni ya Usafi SUMAJKT Cleaning and Fumigation kwa huduma nzuri wanayotoa. 

Katika mahojiano na SUMAJKT TV tarehe 09 April 2022 Meneja Mayira alisema  kuwa SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co. Limited wanatoa huduma nzuri kituoni hapo kutokana na kuwa na Watendaji wa kutosha pamoja na vitendea kazi vya kutosha tofauti na makampuni mengine ambapo mwanzoni huleta wafanyakazi wengi na baadae hupungua na eneo la kufanya usafi ni kubwa.


Aidha ameeleza kuwa Uongozi wa Mbezi Luis Bus Terminal umekuwa ukishirikiana na kampuni hiyo katika kuhakikisha jukumu hilo linatimizwa ipasavyo.

Meneja Mayira amezisihi kampuni zingine za usafi kuiga mfano kwa SUMAJKT.


SUMAJKT Cleaning and Fumigation Company Limited ni kampuni tanzu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) iliyojizatiti katika utoaji wa huduma ya usafi na unyunyiziaji dawa.

 Kampuni imejizatiti katika utoaji wa huduma za usafi katika maeneo yafuatayo:


a. Usafi wa maofisini 

b. Usafi wa sakafu za                       majengo makubwa 

c. Usafi wa kapeti 

d. Usafi wa hospitali 

e. Usafi wa sokoni 

f. Usafi wa barabara 

g. Uzoaji taka 

h. Upandaji miti 

i.  Utunzaji wa bustani na sehemu za kupikia


Kurudisha muonekano uliopotea kuwa wa kuvutia, kama eneo lako linakosa muonekano mzuri na wakuvutia, sinki na dishi za kunawia mikono ikiwa zimepoteza muonekano wake Kampuni ya SUMAJKT Cleaning and Fumigation ipo kwa ajili ya kurudisha mwonekano mzuri wa mazingira yako.


Kampuni katika upande wa Unyunyiziaji dawa inatoa huduma kutegemeana na aina tofauti za vimelea na wadudu wa aina tofauti ambapo dawa na kemikali hutumika kwenye unyunyiziaji. 


Aina zote za dawa za unyunyiziaji kwa wadudu na vimelea ni sumu hatari kwa afya ya binadamu na wanyama.


Hivyo inashauriwa kutumia wataalamu wenye leseni zilizothibitishwa na mamlaka ya dawa na unyunyiziaji kufanya kazi hiyo.


Aidha Kampuni ina uzoefu wa kazi za usafi na unyunyiziaji dawa kwa wateja mbali mbali ikiwa na wataalamu na vifaa bora vya kisasa na imejizatiti kufanya kazi hii kwa umakini na usalama wa hali ya juu, hivyo kuwa kampuni sahihi ya usafi na unyunyiziaji dawa wa eneo lako.

Kampuni inatoa huduma ya unyunyiziaji dawa katika:


a. Mahoteli 

b. Maofisini 

c. Hospitali 

d. Migahawa 

e. Maghala 

f.  Makontena 

g. Vyuoni 

h. Majumbani 

i.  Bustani 

j.  Dawa za nafaka 


Karibuni kwa huduma bora zinazotolewa kwa viwango vya juu, Ofisi zetu zipo Mwenge mkabala na Efatha Ministry Dar es Salaam Tanzania. 


Kwa mawasiliano zaidi tunapatikana kwa simu namba +255734281585/+255712659139 au 

barua pepe :sumajktcleaning@gmail.com au info@sumajkt.go.tz

Tovuti: www.sumajkt.go.tz

Karibuni .



Comments

Popular posts from this blog

UJUE MRADI WA UFUGAJI SAMAKI KWA KUTUMIA MATENKI- SUMAPONICS

 Katika video ni  mradi wa ufugaji wa samaki sato  unaojulikana kwa jina la SUMAPONICS uliopo  Mbweni JKT Dar es Salaam Tanzania.  Huu ni mradi mmojawapo kati ya miradi mingi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT). SUMAJKT Tv imetembelea mradi huo 11 March 2022 na kupata kuzungumza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa mradi huo , na wengine kama inavyoonekana hapo. UFUGAJI SAMAKI WA MATENKI KWA KUZUNGUSHA MAJI (RE – CIRCULATION  AQUACULTURE SYSTEM – RAS) MBWENI JKT Ufugaji wa samaki kwa njia za mabwawa unahitaji rasilimali nyingi hasa ardhi, maji mengi na nguvu kazi kubwa ili kupelekea njia ya ufugaji samaki kwa matenki kwa kuzungusha maji (Recirculating Aquaculture System- RAS). RAS NI NINI? RAS ni mfumo wa kufuga samaki kwa kuzungusha maji ili kutoa uchafu pamoja na kuwaongezea hewa ya ziada samaki waliopo kwenye matenki. RAS ZA SUMAJKT Hizi ni RAS zinazotengenezwa katika mradi wa SUMAPONICS ambazo zina uwezo wa kutoa samaki wenye uzito...

“NAENDELEZA KAZI NINAZOZIJUA”- MEJA JENERALI MABELE

 Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT ) Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele tarehe 19/5/2022 ametimiza mwaka Mmoja madarakani huku akiendelea kutekeleza vema  azma ya Jeshi la Kujenga Taifa kujilisha pamoja na malezi ya vijana. Aidha tarehe 19 Mei 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alimteua kwa kipindi hicho akiwa  Brigedia Jenerali Rajabu Nduku Mabele kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afsa mtendaji mkuu wa SUMAJKT  Hatua iliyokuja kufuatia  aliyekuwa Mkuu wa Jeshi hilo, Meja Jenerali Charles Mbuge kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera akichukua nafasi ya Brig Jenerali Marco Elisha Gaguti aliyehamishiwa Mtwara. katika kipindi cha Mwaka mmoja akiwa madarakani Meja Jenerali Mabele ameendelea kutekeleza Majukumu yake kwa weledi ikiwa ni pamoja na kuliongoza vema Jeshi la Kujenga Taifa na Shirika lake la Uzalishaji Mali S...