Katika mahojiano na SUMAJKT TV tarehe 09 April 2022 Meneja Mayira alisema kuwa SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co. Limited wanatoa huduma nzuri kituoni hapo kutokana na kuwa na Watendaji wa kutosha pamoja na vitendea kazi vya kutosha tofauti na makampuni mengine ambapo mwanzoni huleta wafanyakazi wengi na baadae hupungua na eneo la kufanya usafi ni kubwa.
Aidha ameeleza kuwa Uongozi wa Mbezi Luis Bus Terminal umekuwa ukishirikiana na kampuni hiyo katika kuhakikisha jukumu hilo linatimizwa ipasavyo.
Meneja Mayira amezisihi kampuni zingine za usafi kuiga mfano kwa SUMAJKT.
SUMAJKT Cleaning and Fumigation Company Limited ni kampuni tanzu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) iliyojizatiti katika utoaji wa huduma ya usafi na unyunyiziaji dawa.
Kampuni imejizatiti katika utoaji wa huduma za usafi katika maeneo yafuatayo:
a. Usafi wa maofisini
b. Usafi wa sakafu za majengo makubwa
c. Usafi wa kapeti
d. Usafi wa hospitali
e. Usafi wa sokoni
f. Usafi wa barabara
g. Uzoaji taka
h. Upandaji miti
i. Utunzaji wa bustani na sehemu za kupikia
Kurudisha muonekano uliopotea kuwa wa kuvutia, kama eneo lako linakosa muonekano mzuri na wakuvutia, sinki na dishi za kunawia mikono ikiwa zimepoteza muonekano wake Kampuni ya SUMAJKT Cleaning and Fumigation ipo kwa ajili ya kurudisha mwonekano mzuri wa mazingira yako.
Kampuni katika upande wa Unyunyiziaji dawa inatoa huduma kutegemeana na aina tofauti za vimelea na wadudu wa aina tofauti ambapo dawa na kemikali hutumika kwenye unyunyiziaji.
Aina zote za dawa za unyunyiziaji kwa wadudu na vimelea ni sumu hatari kwa afya ya binadamu na wanyama.
Hivyo inashauriwa kutumia wataalamu wenye leseni zilizothibitishwa na mamlaka ya dawa na unyunyiziaji kufanya kazi hiyo.
Aidha Kampuni ina uzoefu wa kazi za usafi na unyunyiziaji dawa kwa wateja mbali mbali ikiwa na wataalamu na vifaa bora vya kisasa na imejizatiti kufanya kazi hii kwa umakini na usalama wa hali ya juu, hivyo kuwa kampuni sahihi ya usafi na unyunyiziaji dawa wa eneo lako.
Kampuni inatoa huduma ya unyunyiziaji dawa katika:
a. Mahoteli
b. Maofisini
c. Hospitali
d. Migahawa
e. Maghala
f. Makontena
g. Vyuoni
h. Majumbani
i. Bustani
j. Dawa za nafaka
Karibuni kwa huduma bora zinazotolewa kwa viwango vya juu, Ofisi zetu zipo Mwenge mkabala na Efatha Ministry Dar es Salaam Tanzania.
Kwa mawasiliano zaidi tunapatikana kwa simu namba +255734281585/+255712659139 au
barua pepe :sumajktcleaning@gmail.com au info@sumajkt.go.tz
Tovuti: www.sumajkt.go.tz
Karibuni .
Comments
Post a Comment