Skip to main content

Posts

Showing posts with the label Jitegemee Sekondari

MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA) KUTOA MILIONI ISHIRINI NA TISA KUKARABATI MADARASA JITEGEMEE SEKONDARI

Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Alphayo Kidato ameahidi kutoa kiasi cha milioni ishirini na tisa za kitanzania kwa ajili yakukarabati Madarasa pamoja na Mabweni ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT iliyopo Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam. Ahadi hiyo imetolewa leo tarehe 29 Octoba 2022 na Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Richard Kayombo kwa niaba ya Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Alphayo Kidato aliyemwakilisha katika mahafali hayo ya 38 ya kidato cha nne 2022. Kayombo alitoa shukrani za pongezi kwa uongozi wa shule ya Jitegemee kwa kuona umuhimu wa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa sehemu ya familia ya Jitegemee katika mahafali ya 38 ya wanafunzi wa kidato cha nne. Pia Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Richard Kayombo amewasihi wahitimu na wanafunzi wengine kuhakikisha wanaongeza nidhamu katika masomo ili w

MAISHA NI MAPAMBANO - Meja Misigaro

  NAIBU Kamanda Kikosi cha Mgulani JKT, Meja Eusebius Misigaro amewakumbusha Wanafunzi wahitimu wa mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo katika shule ya Sekondari ya Jitegemee kuwa Maisha ni mapambano ambayo yanahitaji maandalizi mazuri na njia sahihi ya kujiandaa kupata Elimu, maarifa, fikra na ujuzi sahihi. Meja Misigaro ameyasema hayo leo tarehe 21 Oktoba 2022 alipokuwa akifunga mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo kwa Wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka 2022/2023 na wahamiaji wa kidato cha kwanza na kidato cha tatu. Mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo wanayopatiwa wanafunzi wanaoanza Shule katika shule ya Sekondari Jitegemee yana dhima Kuu ambayo ni kumjenga Mwanafunzi na kimaadili ili elimu anayopata iweze kumsaidia kikamilifu katika kupambana na changamoto mbalimbali za maisha ya kila siku sambamba na mwanafunzi kuwa na nidhamu na maadili mema, kwani nidhamu ni msingi wa mafanikio katika maisha.  Elimu ya darasani ni vema iende sambamba na kupandikiza chembechembe za nidhamu Kwa mwanafunz

MJIEPUSHE NA MAKUNDI YASIYOFAA-MEJA MWAKALEBE

  Kaimu Kamanda Kikosi Mgulani JKT Meja Heri Mwakalebe amewahasa wanafunzi wa kidato cha kwanza na waliohamia shule hiyo kuepusha na makundi yasiyofaa ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao. Meja Mwakalebe ameyasema hayo leo tarehe 4 Machi 2022, akiwa Mgeni Rasmi  katika ufungaji wa mafunzo ya ukakamavu na uzalendo kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na wanafunzi waliohamia katika Shule ya Sekondari ya Jitegemee jijini Dar es Salaam. "Wanafunzi acheni kujihusisha na makundi yasiofaa ili kujiepusha kuingia katika vishawishi vya matumizi mabaya ya dawa za kulevya na tabia nyingine zisizofaa" alisema Meja Mwakalebe. Meja Mwakalebe amewataka wanafunzi hao kutumia muda wao kusoma ili kutimiza ndoto za maisha yao kwa kupata elimu bora ili kupambana na adui ujinga ambaye ni chanzo cha maradhi na umaskini. Vilevile, amewahimiza wanafunzi wa kike kujiepusha na vishawishi mbalimbali badala yake wajifunze kutoka kwa wanawake waliofanikiwa na kufanya vizuri kwa kuwa viongozi katika T