Kanali Petro Ngata, amefanya ziara hiyo jana tarehe 22 Julai 2022 alipotembelea miradi mbali mbali ya ujenzi katika mji wa serikali Mtumba , Shule ya Mfano Iyumbu pamoja ukaguzi wa mitambo katika kiwanda cha mabati SUMAJKT Roofing Company Limited kilichopo Dodoma.
Pia amekagua maendeleo ya Ujenzi wa jengo la wizara ya Katiba na Sheria, unaotekelezwa na SUMAJKT Construction Company Limited Ujenzi kanda ya Mashariki,
Pia amekagua Ujenzi wa jengo la Mwanasheria Mkuu wa Serikali unaotekelezwa na SUMAJKT ujenzi Kanda ya Kati Dodoma, Ujenzi wa Jengo la Wakili Mkuu wa Serikali unaotekelezwa na SUMAJKT Makao Makuu, Ujenzi wa Jengo la Wakala wa Mtandao wa Serikali, Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya waziri mkuu, jengo la Sera,
Ujenzi wa jengo la ofisi ya Waziri Mkuu jengo la Kazi na Ajira
na Ujenzi wa jengo la wizara ya Kilimo unaotekelezwa na ujenzi kanda ya nyanda za juu kusini,
Ujenzi wa jengo la Ofisi ya Makamu wa Rais jengo la Mazingira na Muungano unaotekelezwa na ujenzi Makao makuu.
Kanali Ngata, alihitimsha ukaguzi wa miradi hiyo kwa kukagua Ujenzi wa Shule ya Mfano (Model School) iliyopo Iyumbu ambapo mradi huo unaotekelezwa na ujenzi kanda ya Kati.
Aidha, Kanali Petro Ngata, ameridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa katika miradi hiyo na amewataka watendaji kuendeleza ubora katika kazi na mahusiano mazuri na washitiri na pia kuendelea kutumia ushauri elekezi wa washauri majenzi (Consultancy)
Kanali Ngata, alihitimisha ziara hiyo kwa kutembelea kiwanda cha mabati SUMAJKT Roofing Company Limited kilichopo Medel Mashariki Jijini Dodoma na kukagua mitambo ya utengenezaji mabati na misumari.
SUMAJKT imekuwa ikipokea miradi mbali mbali kutoka taasisi za serikali na binafsi na kukamilisha kwa wakati.
Comments
Post a Comment