Skip to main content

Posts

Showing posts with the label SUMAJKT Construction Company Ltd

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalisahaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo ya kukamilishwa kwa wakati miradi ya ujenzi inayojengwa na Mkandarasi SUMAJKT Construction Co. Ltd Kanda ya Ziwa.  Kanali Petro Ngata akiendelea na ziara katika miradi ya ujenzi kanda ya ziwa, ametembelea  Ujenzi wa majengo ya OPD, RCH, Pharmacy na Mortuary yaliyopo katika Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza.  Aidha Kanali Ngata ameagiza kasi ya ujenzi iongezwe na ifanyike kwa njia ya oparesheni ambapo majengo ya "Pharmacy" na "Mortuary" yawe yamekamilika ifikapo tarehe 30 Nov 22 na "OPD" na "RCH" yakamilike ifikapo tarehe 12 Dec 22.  Vile vile Kanali Ngata amepata wasaa wa kutembelea Jengo la Halmashauri ya Bunda na kuagiza Meneja Ujenzi Kanda ya Ziwa kumuandikia Mshauri wa Mradi changamoto zote zinazosababisha ucheleweshaji wa mradi huu unaotekelezwa kwa njia ya "Force Account" ili uweze kukamilika kwa w

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MRADI WA UJENZI MTUMBA KUKAMILIKA KWA WAKATI-KANALI PETRO NGATA

Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata amesema mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba unaotekelezwa na kampuni  tanzu ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited (SCCL) utakamilika kwa wakati uliopangwa. Kanali Petro Ngata amesema hayo jana (Jumatatu, Septemba 5, 2022) wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika kukagua maendeleo ujenzi wa Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.  "Mheshimiwa Waziri Mkuu ameridhishwa sana na kazi tunazozifanya hapa katika mji wa serikali Sisi  SUMAJKT tunatekeleza miradi idadi tisa kwa maana ya majengo ya wizara na yote yapo katika hatua nzuri na tunakwenda na wakati kulingana na mkataba ulivyo.  Na sisi kama SUMAJKT kwa kuzingatia maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri Mkuu siku hii ya leo tumejipanga kuhakikisha kwamba tunakamilisha hili jukumu katika muda aliopanga Mheshimiwa Waziri Mkuu."alisema Kanali Ngata.   Nae Meneja wa Ujenzi SUMAJKT-Kanda ya Magharibi Kanali Mbaraka Magogo amesema kuwa mr

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMEAGA KAYA ZINGINE 25 NGORO NGORO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameaga kaya zingine 25, zenye watu 105, na amesema mpaka kufikia tarehe 18/8/2022,  jumla ya kaya 1,002 zenye watu 5,382 zimejiandikisha kwa hiari kuhama katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro na kuelekea kijiji cha Msomera wilayani Handeni mkoa wa Tanga,  lililotengwa na serikali kwa ajili ya wakazi hao. Kati ya kaya hizo,  tayari kaya 624 zenye watu 3,323 zimehakikiwa na kufanyiwa uthamini na kati ya kaya hizo, kaya 106 zenye watu 536 zimeshahamia kijiji cha Msomera wilayani Handeni Mkoani Tanga. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema hayo Agosti 19,2022 Mkoani Arusha sambamba na zoezi la kukabidhi hundi ya Malipo kwa wakazi wapya wa Msomera. Hafla fupi ilifanyika kwenye ofisi za mamlaka ya hifadhi  hiyo kwa nia ya kufanikisha hatua hiyo. Aidha , Mhe. Kassim Majaliwa ameeleza kuwa, Rais Samia Suluhu Hassan amepongeza uamuzi wa wananchi hao na kwamba serikali itaendelea kuwekeza katika kuboresha miundombinu ya eneo la Msomera.  “Napenda kumhakikishia Mheshimiwa

ZINGATIENI UBORA KATIKA MIRADI YA UJENZI-KANALI NGATA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amekagua Miradi tisa ya ujenzi jijini Dodoma inayojengwa na SUMAJKT Construction Company Ltd, kupitia Kanda mbali mbali. Kanali Petro Ngata, amefanya ziara hiyo jana tarehe 22 Julai 2022 alipotembelea  miradi mbali mbali ya ujenzi katika mji wa serikali Mtumba , Shule ya Mfano Iyumbu pamoja ukaguzi wa mitambo katika kiwanda cha mabati SUMAJKT Roofing Company Limited kilichopo Dodoma. Pia amekagua maendeleo ya Ujenzi wa jengo la wizara ya Katiba na Sheria, unaotekelezwa na SUMAJKT Construction Company Limited Ujenzi kanda ya Mashariki,    Pia amekagua Ujenzi wa jengo la Mwanasheria Mkuu wa Serikali unaotekelezwa na  SUMAJKT ujenzi Kanda ya Kati Dodoma, Ujenzi wa Jengo la Wakili Mkuu wa Serikali  unaotekelezwa na SUMAJKT  Makao Makuu, Ujenzi wa Jengo la Wakala wa Mtandao wa Serikali, Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya waziri mkuu, jengo la  Sera,  Ujenzi wa jengo la ofisi ya Waziri Mkuu jen

SUMAJKT YAKABIDHIWA MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA JAMII YA WAKAZI KUTOKA NGORO NGORO

Taasisi ya Hifadhi ya Ngorongoro ( Ngoro ngoro Conservation Area Authority ( NCAA)  imekabidhi Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga  Taifa ( SUMAJKT) Mradi wa Ujenzi wa nyumba 400 eneo la  Msomela mkoani Tanga kwa  ajili ya Makazi ya jamii ya kimasai kutoka  Ngorongoro mkoani Arusha. Akikabidhiwa Mradi huo tarehe 21 Juni 2022, Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT kanali Petro Ngata amesema kuwa, SUMAJKT ipo tayari kukamilisha kazi hiyo kwa wakati  na kwa ufanisi.                                       "Shirika hili limekuwa likipokea kazi mpya na zilizoshindwa na kampuni nyingine  na kuzikamilisha kwa weledi wa hali ya juu"alisema Kanali Ngata. Nae Mhandisi Joshua Mwankunda kutoka NCAA amesema tayari wamekwisha kamilisha mahitaji muhimu ya awali ikiwemo Michoro, Barabara, Shule, mipaka pamoja na njia za mawasiliano. Mhandisi Joshua ameeleza kuwa tathmini ya mradi huo inaonesha Utagharimu Fedha za Kitanzania Shilingi Bilioni Tisa(9). "Tunaimani kubwa na SUMAJKT kwa ute

SUMAJKT YAKABIDHIWA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA USAFISHAJI FIGO LUGALO

Kampuni ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited imekabidhiwa eneo  kwa ajili ya  Ujenzi wa Jengo la Usafishaji Figo, Ukumbi wa mkutano na Jengo la Uchunguzi wa magonjwa Lugalo  jijini Dar es Salaam.  Makabidhiano hayo yamefanyika  tarehe 11 machi 2022, ambapo maandalizi ya usafishaji wa eneo hilo la Ujenzi yameanza siku hiyo.  Eneo hilo litajengwa Ukumbi wa mkutano, Jengo la Uchunguzi wa magonjwa pamoja na Jengo dogo la  wagonjwa baada ya matibabu. Aidha lengo la mradi huo ni kuboresha huduma za Usafishaji Figo (Dialysis) na huduma nyingine zinazotolewa katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.  SUMAJKT kupitia Kampuni yake ya Ujenzi (SUMAJKT Construction Company Ltd) imeanza utekelezaji wa Ujenzi wa Miradi hiyo ambayo kukamilika ndani ya miezi sita. SUMAJKT kupitia Kampuni yake ya Ujenzi (SUMAJKT  Construction Company Ltd) imekuwa ikiaminiwa kwa kukabidhiwa miradi mbalimbali ya Ujenzi na Serikali pamoja na Taasisi binafsi kwa sababu ya kukamilisha Miradi hiyo k