Skip to main content

Posts

MJIEPUSHE NA MAKUNDI YASIYOFAA-MEJA MWAKALEBE

  Kaimu Kamanda Kikosi Mgulani JKT Meja Heri Mwakalebe amewahasa wanafunzi wa kidato cha kwanza na waliohamia shule hiyo kuepusha na makundi yasiyofaa ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao. Meja Mwakalebe ameyasema hayo leo tarehe 4 Machi 2022, akiwa Mgeni Rasmi  katika ufungaji wa mafunzo ya ukakamavu na uzalendo kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na wanafunzi waliohamia katika Shule ya Sekondari ya Jitegemee jijini Dar es Salaam. "Wanafunzi acheni kujihusisha na makundi yasiofaa ili kujiepusha kuingia katika vishawishi vya matumizi mabaya ya dawa za kulevya na tabia nyingine zisizofaa" alisema Meja Mwakalebe. Meja Mwakalebe amewataka wanafunzi hao kutumia muda wao kusoma ili kutimiza ndoto za maisha yao kwa kupata elimu bora ili kupambana na adui ujinga ambaye ni chanzo cha maradhi na umaskini. Vilevile, amewahimiza wanafunzi wa kike kujiepusha na vishawishi mbalimbali badala yake wajifunze kutoka kwa wanawake waliofanikiwa na kufanya vizuri kwa kuwa viongozi katika T

SUMAJKT YAKABIDHI HUNDI KUSAIDIA KUTANGAZA LUGHA YA KISWAHILI

Kaimu naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Kanali Shija Lupi amekabidhi hundi ya zaidi ya Milioni moja na laki nane (1,800,000/=) kwa Bwana Issack Kalumba ambaye anaendesha baiskeli katika nchi mbalimbali Barani Afrika kwa lengo la kuinua na kutangaza lugha ya kiswahili pamoja na utalii wa Tanzania kupitia majukwaa rasmi katika nchi hizo. Kanali Lupi alikabidhi hundi hiyo kwa Bwana Kalumba tarehe 04 March 2022 ofisini kwake Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa jijini Dar es salaam. SUMAJKT imetoa hundi ya kiasi hicho cha pesa kuunga mkono juhudi za Bwana Isaack Kalumba  ambaye alileta maombi SUMAJKT la kusaidiwa fedha hizo ili kuweza kutatua baadhi ya changamoto anazokutana nazo katika mzunguko wa Safari yake ya kuinua na kutangaza lugha ya kiswahili Barani Afrika. Bwana Isaack Kalumba ni Mtanzania anaeendesha baiskeli katika nchi mbalimbali Barani Afrika kwa lengo la kuinua na kuitangaza lugha ya kiswahili Afrika na kuunga mkono juhu

SUMAJKT GUARD LTD WAHITIMU MAFUNZO YA ISO

  Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Shija Lupi, amewataka wahitimu wa mafunzo ya uandaaji wa nyaraka kwa mujibu wa kiwango cha ubora (ISO 9001:2015) kufanya kazi kwa weledi na kuwa tayari kutoa elimu waliyoipata kwa wengine ambao hawakubahatika kuhudhuria mafunzo hayo.  Kanali Shija Lupi,  amezungumza hayo tarehe 11 Machi 2022 wakati  akifunga mafunzo ya ISO kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata, katika ukumbi wa mkutano Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. "Endeleeni kujifunza ili kuongeza tija ya Utendaji kazi ndani ya shirika la Uzalishaji Mali (SUMAJKT )".alisema Kanali Lupi Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Ulinzi SUMAJKT Guard Ltd,  Kanali Joseph Masanja, amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele, kwa kukubali kuendeshwa kwa mafunzo hayo.  Kanali Joseph Masanja, amefafanu

SUMAJKT YAKABIDHIWA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA USAFISHAJI FIGO LUGALO

Kampuni ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited imekabidhiwa eneo  kwa ajili ya  Ujenzi wa Jengo la Usafishaji Figo, Ukumbi wa mkutano na Jengo la Uchunguzi wa magonjwa Lugalo  jijini Dar es Salaam.  Makabidhiano hayo yamefanyika  tarehe 11 machi 2022, ambapo maandalizi ya usafishaji wa eneo hilo la Ujenzi yameanza siku hiyo.  Eneo hilo litajengwa Ukumbi wa mkutano, Jengo la Uchunguzi wa magonjwa pamoja na Jengo dogo la  wagonjwa baada ya matibabu. Aidha lengo la mradi huo ni kuboresha huduma za Usafishaji Figo (Dialysis) na huduma nyingine zinazotolewa katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.  SUMAJKT kupitia Kampuni yake ya Ujenzi (SUMAJKT Construction Company Ltd) imeanza utekelezaji wa Ujenzi wa Miradi hiyo ambayo kukamilika ndani ya miezi sita. SUMAJKT kupitia Kampuni yake ya Ujenzi (SUMAJKT  Construction Company Ltd) imekuwa ikiaminiwa kwa kukabidhiwa miradi mbalimbali ya Ujenzi na Serikali pamoja na Taasisi binafsi kwa sababu ya kukamilisha Miradi hiyo k