Skip to main content

SUMAJKT YAKABIDHI HUNDI KUSAIDIA KUTANGAZA LUGHA YA KISWAHILI


Kaimu naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Kanali Shija Lupi amekabidhi hundi ya zaidi ya Milioni moja na laki nane (1,800,000/=) kwa Bwana Issack Kalumba ambaye anaendesha baiskeli katika nchi mbalimbali Barani Afrika kwa lengo la kuinua na kutangaza lugha ya kiswahili pamoja na utalii wa Tanzania kupitia majukwaa rasmi katika nchi hizo.


Kanali Lupi alikabidhi hundi hiyo kwa Bwana Kalumba tarehe 04 March 2022 ofisini kwake Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa jijini Dar es salaam.


SUMAJKT imetoa hundi ya kiasi hicho cha pesa kuunga mkono juhudi za Bwana Isaack Kalumba  ambaye alileta maombi SUMAJKT la kusaidiwa fedha hizo ili kuweza kutatua baadhi ya changamoto anazokutana nazo katika mzunguko wa Safari yake ya kuinua na kutangaza lugha ya kiswahili Barani Afrika.


Bwana Isaack Kalumba ni Mtanzania anaeendesha baiskeli katika nchi mbalimbali Barani Afrika kwa lengo la kuinua na kuitangaza lugha ya kiswahili Afrika na kuunga mkono juhudi za Serikali za kukuza na kuzungumza lugha ya kiswahili katika nchi za kiafrika.


Pia bwana Kalumba tangu aanze harakati za kutangaza kiswahili tarehe 21Oktoba 2021 Jijini Dar es salaam, ameweza kupita nchi kadhaa zikiwemo Kenya, Sudani Kusini, Uganda na Rwanda ambapo anatangaza lugha ya kiswahili kupitia majukwaa rasmi, Taasisi mbalimbali, Mashirika, Vyuo vikuu na shule mbalimbali.


Bwana Isaack Kalumba amelishukuru Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kwa kumpatia fedha hizo na kuahidi kuendelea kushirikiana na SUMAJKT katika harakati zake za kuinua na kutangaza lugha ya kiswahili ambapo kwasasa anajiandaa na safari ya kuelekea nchi za Malawi, Zambia, Zimbabwe, Botswana na nchini Afrika Kusini.

Comments

Popular posts from this blog

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.