Kampuni ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited imekabidhiwa eneo kwa ajili ya Ujenzi wa Jengo la Usafishaji Figo, Ukumbi wa mkutano na Jengo la Uchunguzi wa magonjwa Lugalo jijini Dar es Salaam.
Makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 11 machi 2022, ambapo maandalizi ya usafishaji wa eneo hilo la Ujenzi yameanza siku hiyo.
Eneo hilo litajengwa Ukumbi wa mkutano, Jengo la Uchunguzi wa magonjwa pamoja na Jengo dogo la
wagonjwa baada ya matibabu.
Aidha lengo la mradi huo ni kuboresha huduma za Usafishaji Figo (Dialysis) na huduma nyingine zinazotolewa katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.
SUMAJKT kupitia Kampuni yake ya Ujenzi (SUMAJKT Construction Company Ltd) imeanza utekelezaji wa Ujenzi wa Miradi hiyo ambayo kukamilika ndani ya miezi sita.
SUMAJKT kupitia Kampuni yake ya Ujenzi (SUMAJKT Construction Company Ltd) imekuwa ikiaminiwa kwa kukabidhiwa miradi mbalimbali ya Ujenzi na Serikali pamoja na Taasisi binafsi kwa sababu ya kukamilisha Miradi hiyo katika ubora na wakati.
Comments
Post a Comment