Skip to main content

MRADI WA UJENZI MTUMBA KUKAMILIKA KWA WAKATI-KANALI PETRO NGATA



Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata amesema mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba unaotekelezwa na kampuni 

tanzu ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited (SCCL) utakamilika kwa wakati uliopangwa. Kanali Petro Ngata amesema hayo jana (Jumatatu, Septemba 5, 2022) wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika kukagua maendeleo ujenzi wa Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.

 "Mheshimiwa Waziri Mkuu ameridhishwa sana na kazi tunazozifanya hapa katika mji wa serikali Sisi 
SUMAJKT tunatekeleza miradi idadi tisa kwa maana ya majengo ya wizara na yote yapo katika hatua nzuri na tunakwenda na wakati kulingana na mkataba ulivyo. 


Na sisi kama SUMAJKT kwa kuzingatia maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri Mkuu siku hii ya leo tumejipanga kuhakikisha kwamba tunakamilisha hili jukumu katika muda aliopanga Mheshimiwa Waziri Mkuu."alisema Kanali Ngata. 


 Nae Meneja wa Ujenzi SUMAJKT-Kanda ya Magharibi Kanali Mbaraka Magogo amesema kuwa mradi huo umefikia asilimia 46 na upo ndani ya muda wa mkataba. Aidha, Kanali Magogo amesema kuwa
kazi hizo wanatarajia kuzikamilisha tarehe 9 Septemba 22. Nae Meneja wa Ujenzi SUMAJKT Kanda ya Kati Meja Samwel Jambo amesema " Malengo ifikapo mwezi Novemba mwaka huu ujenzi wa jengo kwa ujumla tuanze kazi ya finishing, ambayo inahusisha 
plasta pamoja na kazi zingine zote za finishing, kwa hiyo tunatarajia miezi kumi ijayo baada ya kukamilisha tutakuwa tunapambana na umaliziaji. 

 Vile vile Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni hiyo ya Ujenzi SCCL Mhandisi Morgan Nyonyi ameahidi kuwa wao kama Wakandarasi daraja la kwanza katika mradi huo watatekeleza maelekezo yaliyotolewa na Mhe Waziri Mkuu na sambamba na ujenzi wa majengo hayo. Miradi yote ya ujenzi inayotekelezwa na SUMAJKT inagharimu Tsh bilioni 150.


 

Comments

Popular posts from this blog

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup

MHESHIMIWA BASHUNGWA ALIPONGEZA JKT

  Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Innocent Bashungwa amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kwa kuendelea kutekeleza jukumu la malezi ya Vijana kupitia mafunzo yao ya Kujitolea na Mujibu wa Sheria yanayotolewa kwenye makambi ya JKT ili kuwajengea uzalendo pamoja na stadi za kazi na waweze kushiriki ujenzi wa Taifa. Mhe. Bashungwa amesema hayo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kujitambulisha, Makao Mkuu ya JKT Chamwino, Jijini Dodoma ambapo alipata fursa ya kuongea na Maafisa, Askari, Vijana na Watumishi wa Umma wanaofanyia kazi JKT eneo la Dodoma. Mhe. Bashungwa ameongeza kuwa, Kukamilika kwa miradi ya Kilimo cha kimkakati katika shamba la SUMAJKT lililopo Mngeta na Ujenzi wa miundombinu ya Skimu ya Umwagiliaji iliyopo katika kikosi cha Chita JKT mkoani Morogoro, Italeta tija katika upatikanaji wa chakula cha kutosha na kulihakikishia Taifa Usalama wa Chakula pamoja na upatikanaji wa Mbegu bora. Ameongeza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita imetenga bajeti ya fedha kupitia Wizara ya U

MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA) KUTOA MILIONI ISHIRINI NA TISA KUKARABATI MADARASA JITEGEMEE SEKONDARI

Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Alphayo Kidato ameahidi kutoa kiasi cha milioni ishirini na tisa za kitanzania kwa ajili yakukarabati Madarasa pamoja na Mabweni ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT iliyopo Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam. Ahadi hiyo imetolewa leo tarehe 29 Octoba 2022 na Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Richard Kayombo kwa niaba ya Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ndugu Alphayo Kidato aliyemwakilisha katika mahafali hayo ya 38 ya kidato cha nne 2022. Kayombo alitoa shukrani za pongezi kwa uongozi wa shule ya Jitegemee kwa kuona umuhimu wa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa sehemu ya familia ya Jitegemee katika mahafali ya 38 ya wanafunzi wa kidato cha nne. Pia Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndugu Richard Kayombo amewasihi wahitimu na wanafunzi wengine kuhakikisha wanaongeza nidhamu katika masomo ili w