Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata amesema mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba unaotekelezwa na kampuni
tanzu ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited (SCCL) utakamilika kwa wakati uliopangwa. Kanali Petro Ngata amesema hayo jana (Jumatatu, Septemba 5, 2022) wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika kukagua maendeleo ujenzi wa Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.
"Mheshimiwa Waziri Mkuu ameridhishwa sana na kazi tunazozifanya hapa katika mji wa serikali Sisi
SUMAJKT tunatekeleza miradi idadi tisa kwa maana ya majengo ya wizara na yote yapo katika hatua nzuri na tunakwenda na wakati kulingana na mkataba ulivyo.
Na sisi kama SUMAJKT kwa kuzingatia maelekezo aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri Mkuu siku hii ya leo tumejipanga kuhakikisha kwamba tunakamilisha hili jukumu katika muda aliopanga Mheshimiwa Waziri Mkuu."alisema Kanali Ngata.
Nae Meneja wa Ujenzi SUMAJKT-Kanda ya Magharibi Kanali Mbaraka Magogo amesema kuwa mradi huo umefikia asilimia 46 na upo ndani ya muda wa mkataba. Aidha, Kanali Magogo amesema kuwa
kazi hizo wanatarajia kuzikamilisha tarehe 9 Septemba 22. Nae Meneja wa Ujenzi SUMAJKT Kanda ya Kati Meja Samwel Jambo amesema " Malengo ifikapo mwezi Novemba mwaka huu ujenzi wa jengo kwa ujumla tuanze kazi ya finishing, ambayo inahusisha
plasta pamoja na kazi zingine zote za finishing, kwa hiyo tunatarajia miezi kumi ijayo baada ya kukamilisha tutakuwa tunapambana na umaliziaji.
Vile vile Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni hiyo ya Ujenzi SCCL Mhandisi Morgan Nyonyi ameahidi kuwa wao kama Wakandarasi daraja la kwanza katika mradi huo watatekeleza maelekezo yaliyotolewa na Mhe Waziri Mkuu na sambamba na ujenzi wa majengo hayo. Miradi yote ya ujenzi inayotekelezwa na SUMAJKT inagharimu Tsh bilioni 150.
Comments
Post a Comment