Skip to main content

MHESHIMIWA BASHUNGWA ALIPONGEZA JKT

 



Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Innocent Bashungwa amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kwa kuendelea kutekeleza jukumu la malezi ya Vijana kupitia mafunzo yao ya Kujitolea na Mujibu wa Sheria yanayotolewa kwenye makambi ya JKT ili kuwajengea uzalendo pamoja na stadi za kazi na waweze kushiriki ujenzi wa Taifa.


Mhe. Bashungwa amesema hayo alipofanya ziara ya kikazi iliyolenga kujitambulisha, Makao Mkuu ya JKT Chamwino, Jijini Dodoma ambapo alipata fursa ya kuongea na Maafisa, Askari, Vijana na Watumishi wa Umma wanaofanyia kazi JKT eneo la Dodoma.


Mhe. Bashungwa ameongeza kuwa, Kukamilika kwa miradi ya Kilimo cha kimkakati katika shamba la SUMAJKT lililopo Mngeta na Ujenzi wa miundombinu ya Skimu ya Umwagiliaji iliyopo katika kikosi cha Chita JKT

mkoani Morogoro, Italeta tija katika upatikanaji wa chakula cha kutosha na kulihakikishia Taifa Usalama wa Chakula pamoja na upatikanaji wa Mbegu bora. Ameongeza kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita imetenga bajeti ya fedha kupitia Wizara ya Ulinzi na JKT kwenye Sekta ya kilimo kwa ajili ya ununuzi wa mitambo na zana za kilimo ili kuongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali yakiwemo ya kimkakati kupitia vikosi vya JKT.


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa akifuatilia Taarifa za Shughuli zinazofanywa na Jeshi la Kujenga Taifa Katika Ukumbi wa Mkutano Makao Makuu ya JKT yaliyopo Chamwino Jijini Dodoma.


Mhe. Bashungwa ameeleza kuwa ili Vijana wanaomaliza Mafunzo ya JKT wakalete mabadiliko chanya kiuchumi, ni muhimu kwa JKT, Wizara na Wadau wengine kushirikiana ili kundi hilo kubwa la Vijana wanaomaliza mkataba wa kujitolea wapate ushawishi wa kujiajiri kupitia shughuli za Uzalishaji Mali ikiwemo Kilimo.


Aidha, Mheshimiwa Bashungwa ameushukuru Uongozi wa JKT chini ya Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa maandalizi makubwa ya mapokezi yaliofanyika ambapo amehaidi kushirikiana na JKT katika kutekeleza majukumu mbalimbali chini ya Wizara ya Ulinzi na JKT anayoingoza.


‘’Nakushukuru sana Mkuu wa JKT na timu yako kwa mapokezi mazuri na Taarifa ya Utendaji wa majukumu ya JKT, Mikakati na Changamoto ambayo imenipa picha kamili na uelewa mkubwa wa Utendaji kazi wa JKT’’. Alisema


Naye Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele amempongeza Waziri Bashungwa kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi na JKT na kuahidi kuwa JKT litampa ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza majukumu yake ndani ya JKT.


Kwa upande wake Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema kuwa JKT linatekeleza majukumu yake katika vikosi na makambi yake pamoja na Chuo cha Uongozi cha JKT kilichopo Kimbiji Jijini Dar es Salaam.


  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Innocent Bashungwa akipokea Katika hatua nyingine, Zawadi kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele.


Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Innocent Bashungwa katika ziara hiyo aliyoifanya Makao Makuu ya JKT ameambatana na baadhi ya Wawakilishi wa Wakuu wa Matawi kutoka Makao Makuu ya JWTZ na Wizara ya Ulinzi na JKT pamoja na Wasaidizi kutoka katika ofisi yake.

Comments

Popular posts from this blog

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.