Skip to main content

UJUMBE WA MAAFISA KUTOKA NCHINI ZAMBIA WATEMBELEA SUMAJKT



Ujumbe wa Maafisa kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu nchini Zambia ukiongozwa na Brigedia Jenerali Humphery Nyone leo tarehe 03 Oktoba 2022 umetembelea Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Makao Makuu Mlalakuwa jijini Dar es salaam ili kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT.


Ujumbe huo idadi ya Maafisa 20 umepokelewa na Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Shija Lupi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Elikana Ngata.


Akizungumza mara baada ya kupokea Ugeni huo Kanali Shija Lupi amesema kuwa Zambia na Tanzania zimeendeleza Udugu katika Shughuli mbalimbali za Kibiashara.


"nchi hizi mbili zimekua kiuchumi,  mara baada ya kupata uhuru katika miaka ya 1960,  na Zambia  kwa mara kadhaa imekua ikiagiza bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania,  ikiwemo vifaa vya ujenzi pamoja na mazao ya vyakula,  lakini pia Zambia imekua mzalishaji mkubwa wa bidhaa za kilimo,  kama mahindi,  bidhaa za shaba na nyingine nyingi"


Aidha Kanali Lupi amesema kuwa  katika miundombinu bidhaa nyingi zimekua zikisafirishwa kupitia bandari ya Dar es aaalam  hadi Ndola zaidi ya tani milioni 1, mafuta kupitia Bomba la TAZAMA huku nyingine zikisafirishwa kupitia reli ya TAZARA" alisema Kanali Lupi 


Kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajab Mabele nikushukuru wewe pamoja na ujumbe uliombatana nao,  kwa kuendelea kudumisha Udugu huu.   


Naye,  Meja Athman Levery kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mipango,  Uwekezaji na Utafiti Luteni Kanali George Wang'ombe ameelezea chimbuko la Shirika pamoja na shughuli mbalimbali zinazofanywa kupitia sekta zake nne ambazo ni Ujenzi,  uhandisi na ushauri, sekta ya kilimo ufugaji na uvuvi, 

sekta ya huduma na biadhara pamoja na sekta ya viwanda.


Akielezea sekta ya viwanda amesema kuwa shirika linaboresha viwanda vilivyopo na kuanzisha viwanda vipya. 

“Viwanda vilivyopo ni kiwanda cha cha Ushonaji 

b. Kiwanda cha Samani,  Kiwanda cha Maji ya Kunywa,  Kiwanda cha taa, kiwanda cha mabati na misumari, pamoja na kiwanda cha nafaka” alisema Meja Levery


Aidha Brigedia Jenerali Humphery Nyone alishukuru kwa mapokezi mazuri waliyoyapata Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa jijini Dar es salaam.


Vilevile Brigedia Jenerali Nyone alifurahishwa na shughuli mbalimbali za Uzalishaji Mali zinazofanywa na SUMAJKT ikiwemo Kampuni ya ujenzi, Kilimo, Viwanda pamoja na Ufugaji na kuahidi kuendelea kujifunza kupitia SUMAJKT.

" Tulipokua tunakuja Tz tumeangalia wapi tumetoka Kuanzia kwa baba zetu Keneth Kaunda na Mwl. Nyerere,  Ushirikiano wetu kijeshi una historia, wazo la kuwa na shirika tumelipata hapa na tumeona mnafanya vizuri sana,  kuanzia biashara za aina tofauti na hivyo tunatarajia kuiga mnachokifanya ninyi.


Tunatarajia  pia kushirikiana kwa mambo mengi ndio maana kama chuo tumekuja kujifunza hapa,  pia tunatamani urafiki huu endelee kukua kila uchwao kwani tunategemeana  kiuchumi kupitia reli ya TAZARA.


Endeleeni kufanya mnayofanya   tunazisifu kazi zenu na kila mnachofanya tunaenda kukifanya”

alisema Brigedia Jenerali Nyone .


SUMAJKT imekuwa ikipokea ujumbe kutoka nchi mbali mbali wanaofika kuona shughuli za uzalishaji Mali zinavyoendeshwa na Shirika hilo.

Comments

Popular posts from this blog

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.