Meja Misigaro ameyasema hayo leo tarehe 21 Oktoba 2022 alipokuwa akifunga mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo kwa Wanafunzi wa kidato cha tano kwa mwaka 2022/2023 na wahamiaji wa kidato cha kwanza na kidato cha tatu.
Mafunzo ya Ukakamavu na Uzalendo wanayopatiwa wanafunzi wanaoanza Shule katika shule ya Sekondari Jitegemee yana dhima Kuu ambayo ni kumjenga Mwanafunzi na kimaadili ili elimu anayopata iweze kumsaidia kikamilifu katika kupambana na changamoto mbalimbali za maisha ya kila siku sambamba na mwanafunzi kuwa na nidhamu na maadili mema, kwani nidhamu ni msingi wa mafanikio katika maisha.
Elimu ya darasani ni vema iende sambamba na kupandikiza chembechembe za nidhamu Kwa mwanafunzi, matokeo yake ni mwanafunzi kuwa Mtu bora katika maisha.
Aidha, Meja Misigaro, ametoa rai kwa wahitimu hao kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kama Facebook,Twitter, Whatsapp, Youtube na Instagram kwa ajili ya kujifunza mambo maovu.
Awali akitoa taarifa ya mafunzo hayo Kaimu Mkuu wa Shule Utawala, Meja Dickson Chao amesema mafunzo hayo ya Ukakamavu na Uzalendo yamechukua muda wa majuma mawili ambapo wanafunzi 105 wamehitimu ambapo kati yao wavulana idadi ni 63 na wasichana idadi ni 42.
Wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo Wanafunzi waliohitimu walipita mbele ya mgeni rasmi kwa mwendo wa Pole na mwendo wa Haraka na kisha mgeni rasmi kutoa zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri.
Mafunzo haya ya Ukakamavu na Uzalendo hufanywa kwa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, kidato tano na wanafunzi wanaohamia shuleni hapo kutoka shule nyingine kabla ya kuanza kwa muhula wa masomo ambapo mafunzo hayo ni kama Jando na Unyago, Ili wanafunzi waweze kuendana na mila, kanuni na desturi za shule ya Sekondari Jitegemee.
SUMAJKT inamiliki shule za mbili za sekondari ambazo ni Jitegemee Dar es Salaam na Kawawa iliyopo Mafinga mkoani Iringa.
Comments
Post a Comment