Katika video ni mradi wa ufugaji wa samaki sato
unaojulikana kwa jina la SUMAPONICS uliopo
Mbweni JKT Dar es Salaam Tanzania.
Huu ni mradi mmojawapo kati ya miradi mingi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT).
SUMAJKT Tv imetembelea mradi huo 11 March 2022 na kupata kuzungumza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa mradi huo , na wengine kama inavyoonekana hapo.
UFUGAJI SAMAKI WA MATENKI KWA KUZUNGUSHA MAJI (RE – CIRCULATION
AQUACULTURE SYSTEM – RAS) MBWENI JKT
Ufugaji wa samaki kwa njia za mabwawa unahitaji rasilimali nyingi hasa ardhi, maji mengi na nguvu kazi kubwa ili kupelekea njia ya ufugaji samaki kwa matenki kwa kuzungusha maji (Recirculating Aquaculture System- RAS).
RAS NI NINI?
RAS ni mfumo wa kufuga samaki kwa kuzungusha maji ili kutoa uchafu pamoja na kuwaongezea hewa ya ziada samaki waliopo kwenye matenki.
RAS ZA SUMAJKT
Hizi ni RAS zinazotengenezwa katika mradi wa SUMAPONICS ambazo zina uwezo wa kutoa samaki wenye uzito wa gramu 250 – 350 kwa muda wa miezi minne.
RAS hizi hupandwa mbegu za miezi miwili na mteja hufuga samaki kwa muda wa miezi minne.
AINA ZA RAS ZINAZOPATIKANA
1. RAS YA LITA 5000 (Family Package)
Hii ni Ras inayotengenezwa kwa mteja kwa ajili ya chakula nyumbani, huwa na tenki moja lenye ujazo walita 5000, na lina uwezo wa kubeba kg 125 yani idadi ya samaki 500 kwa wakati mmoja. Mfumo huu hupatikana kwa gharama za Tsh 5,500,000/= na huitaji eneo la ukubwa wa Sqm 12.
2. RAS YA LITA 10,000 (Standard Package)
Hii ni Ras inayotengenezwa kwa mteja kwa ajili ya chakula nyumbani na kwa biashara, huwa na tenki moja lenye ujazo wa lita 10,000 na matenki madogo ya mfumo wa kuchuja maji.
Ras hii ina uwezo wa kubeba kg 250 yani idadi ya samaki 1000 kwa wakati mmoja, mfumo huu hupatikana kwa gharama za Tsh 9,500,000/=
3. RAS YA LITA 30,000
Hii ni RAS inayotengenezwa kwa ajili ya ufugaji samaki wa kibiashara, mfumo huu una matenki mawili ya kufugiasamaki yenye ujazo wa lita 10,000 na lita 20,000.
Mfumo huu unaruhusu kuvuna kg 600 kila baada ya miezi miwili, hii ni kutokana kwamba mfugaji atapanda vifaranga 2000 vya miezi miwili katika tenki la lita 10,000 na baada ya miezi miwili atahamisha kwenda kwenye tenki la lita 20,000 kisha baada ya miezi minne ataanza kuvuna kila baada ya miezi miwili. Bei ya mfumo huu ni Tsh 16,000,000/= ukubwa wa eneo ni Sqm 84.
GHARAMA ZA MIFUMO YOTE ZINAHUSISHA
• Ujenzi kamili wa mfumo kasoro kufunika (Shades)
• Mfumo wa kuzungusha maji
• Chakula cha kuanzia (Kg 10)
• Jedwali la chakula cha kulisha
• Mzani mdogo wa kupimia samaki
• Mafunzo ya ufugaji samaki pamoja na huduma za kitaalamu kila mwezi mpaka mteja atakapovuna kwa mara ya kwanza.
• Mbegu ya awali ya vifaranga kulingana na mfumo uliochagua
FAIDA ZA RAS
• Matumizi ya eneo dogo kulinganisha na mabwawa
• Mavuno makubwa katika eneo dogo
• NI rahisi kuhudumia
• Ni mfumo mzuri katika utunzaji wa mazingira
• Gharama zake za ujenzi ni nafuu.
MRADI WA SUMAPONICS
Mradi huu wa ufugaji samaki na utengenezaji wa mifumo ya ufugaji samaki kwenye matenki yenye kuzungusha maji unapatikana jijini Dar es Salaam eneo la MBWENI JKT.
Pamoja na hayo mradi wa SUMAPONICS unajihusisha na:-
• Uuzaji wa vifaranga vilivyokuzwa
• Mafunzo ya ufugaji samaki
• Ujenzi wa mifumo mingine ya ufugaji samaki kama mabwawa na vizimba (Cage)
• Uuzaji wa samaki wa kufuga
“UCHUMI WA VIWANDA KWA AJIRA NA BIASHARA ENDELEVU’’
Kwa mawasiliano zaidi: Tunapatikana kwa namba +255 767 188 066 au Email: sumaponics@sumajkt.go.tz
Pia Tovuti: www. sumajkt.go.tz
Endelea kufuatilia SUMAJKTTanzania.blogspot.com zijazo kwa miradi mbali mbali ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT).
(NB: Bei tajwa zinaweza kubadilika kulingana na hali ya soko, uzalishaji n.k)
Karibuni
Comments
Post a Comment