Skip to main content

UJUE MRADI WA UFUGAJI SAMAKI KWA KUTUMIA MATENKI- SUMAPONICS


 Katika video ni  mradi wa ufugaji wa samaki sato
 unaojulikana kwa jina la SUMAPONICS uliopo 
Mbweni JKT Dar es Salaam Tanzania. 
Huu ni mradi mmojawapo kati ya miradi mingi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT).


SUMAJKT Tv imetembelea mradi huo 11 March 2022 na kupata kuzungumza na Mkurugenzi Mwendeshaji wa mradi huo , na wengine kama inavyoonekana hapo.

UFUGAJI SAMAKI WA MATENKI KWA KUZUNGUSHA MAJI (RE – CIRCULATION 
AQUACULTURE SYSTEM – RAS) MBWENI JKT


Ufugaji wa samaki kwa njia za mabwawa unahitaji rasilimali nyingi hasa ardhi, maji mengi na nguvu kazi kubwa ili kupelekea njia ya ufugaji samaki kwa matenki kwa kuzungusha maji (Recirculating Aquaculture System- RAS).

RAS NI NINI?
RAS ni mfumo wa kufuga samaki kwa kuzungusha maji ili kutoa uchafu pamoja na kuwaongezea hewa ya ziada samaki waliopo kwenye matenki.

RAS ZA SUMAJKT
Hizi ni RAS zinazotengenezwa katika mradi wa SUMAPONICS ambazo zina uwezo wa kutoa samaki wenye uzito wa gramu 250 – 350 kwa muda wa miezi minne.
RAS hizi hupandwa mbegu za miezi miwili na mteja hufuga samaki kwa muda wa miezi minne.


AINA ZA RAS ZINAZOPATIKANA
1. RAS YA LITA 5000 (Family Package)
Hii ni Ras inayotengenezwa kwa mteja kwa ajili ya chakula nyumbani, huwa na tenki moja lenye ujazo walita 5000, na lina uwezo wa kubeba kg 125 yani idadi ya samaki 500 kwa wakati mmoja. Mfumo huu hupatikana kwa gharama za Tsh 5,500,000/= na huitaji eneo la ukubwa wa Sqm 12.

2. RAS YA LITA 10,000 (Standard Package)
Hii ni Ras inayotengenezwa kwa mteja kwa ajili ya chakula nyumbani na kwa biashara, huwa na tenki moja lenye ujazo wa lita 10,000 na matenki madogo ya mfumo wa kuchuja maji.

Ras hii ina uwezo wa kubeba kg 250 yani idadi ya samaki 1000 kwa wakati mmoja, mfumo huu hupatikana kwa gharama za Tsh 9,500,000/=

3. RAS YA LITA 30,000
Hii ni RAS inayotengenezwa kwa ajili ya ufugaji samaki wa kibiashara, mfumo huu una matenki mawili ya kufugiasamaki yenye ujazo wa lita 10,000 na lita 20,000. 
Mfumo huu unaruhusu kuvuna kg 600 kila baada ya miezi miwili, hii ni kutokana kwamba mfugaji atapanda vifaranga 2000 vya miezi miwili katika tenki la lita 10,000 na baada ya miezi miwili atahamisha kwenda kwenye tenki la lita 20,000 kisha baada ya miezi minne ataanza kuvuna kila baada ya miezi miwili. Bei ya mfumo huu ni Tsh 16,000,000/= ukubwa wa eneo ni Sqm 84.

GHARAMA ZA MIFUMO YOTE ZINAHUSISHA
Ujenzi kamili wa mfumo kasoro kufunika (Shades)
Mfumo wa kuzungusha maji
Chakula cha kuanzia (Kg 10)
Jedwali la chakula cha kulisha
Mzani mdogo wa kupimia samaki
Mafunzo ya ufugaji samaki pamoja na huduma za kitaalamu kila mwezi mpaka mteja atakapovuna kwa mara ya kwanza.
Mbegu ya awali ya vifaranga kulingana na mfumo uliochagua

FAIDA ZA RAS
Matumizi ya eneo dogo kulinganisha na mabwawa
Mavuno makubwa katika eneo dogo
NI rahisi kuhudumia 
Ni mfumo mzuri katika utunzaji wa mazingira
Gharama zake za ujenzi ni nafuu.

MRADI WA SUMAPONICS
Mradi huu wa ufugaji samaki na utengenezaji wa mifumo ya ufugaji samaki kwenye matenki yenye kuzungusha maji unapatikana  jijini Dar es Salaam eneo la MBWENI JKT.
Pamoja na hayo mradi wa SUMAPONICS unajihusisha na:-
Uuzaji wa vifaranga vilivyokuzwa
Mafunzo ya ufugaji samaki
Ujenzi wa mifumo mingine ya ufugaji samaki kama mabwawa na vizimba (Cage)
Uuzaji wa samaki wa kufuga

“UCHUMI WA VIWANDA KWA AJIRA NA BIASHARA ENDELEVU’’

Kwa mawasiliano zaidi: Tunapatikana kwa namba +255 767 188 066 au Email: sumaponics@sumajkt.go.tz
Pia Tovuti: www. sumajkt.go.tz 

Endelea kufuatilia SUMAJKTTanzania.blogspot.com  zijazo kwa miradi  mbali mbali ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT).
(NB: Bei tajwa zinaweza kubadilika kulingana na hali ya soko, uzalishaji n.k)
Karibuni

Comments

Popular posts from this blog

SUMAJKT YAKABIDHI VIATU VYA SHULE JOZI 500

 Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kupitia Kampuni tanzu iitwayo SUMAJKT shoes and leather Products Co LTD. tarehe 04 Novemba 2022 limekabidhi viatu vya ngozi jozi 500 kwa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao yenye kauli mbiu “Samia nivike viatu”. Aidha, makabidhiano ya viatu hivyo yamefanyika Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam. Akielezea historia ya kiwanda Mkurugenzi Mwendeshaji wa kiwanda hicho Meja Mathias John amesema, Kiwanda cha  viatu na bidhaa za ngozi SUMAJKT Shoes and Leather Product Co. LTD Kilianzishwa Jul 2017 na majukumu yake yakiwa ni uzalishaji wa viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.  Aidha, toka kuanzishwa Kqa  kiwanda hicho kimeendelea kuongeza uwezo wa uzalishaji kwa kununua vifaa na mashine za kisasa ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.  Bidhaa zinazozalishwa ni viatu kwa ajili ya taasisi za ulinzi, viatu vya usalama (safety boots), viatu vya maofisini na viatu vya shule.  Uwezo wa kiwanda ni kuzalisha viatu jozi 500 kwa siku na Kup

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA MIRADI YA UJENZI KANDA YA ZIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata leo tarehe 28 Oktoba 22 amefanya ziara katika miradi ya ujenzi inayoendelea kujengwa kanda ya ziwa. Kanali Petro Ngata amekagua miradi mbali mbali inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa jengo la uchunguzi (Dignostic Center) katika hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Kahama , Mradi wa uondoaji wa kifusi eneo la hanga uwanja wa ndege wa Chato Mkoani Geita na Mradi wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Msalala. Aidha, Kanali Ngata  amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala kuhusu ukamilishwaji wa  jengo la ofisi za Halmashauri. SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo ina kanda saba za ujenzi.

MKURUGENZI MTENDAJI SUMAJKT KATIKA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata, amehitimisha Ziara yake kwa kutembelea Kikosi cha JKT Mafinga Mkoani Iringa ambapo SUMAJKT katika kikosi hicho imewekeza katika ufugaji wa mifugo mbali mbali ikiwemo ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe. Bonyeza video hiyo kuona yaliyojiri.