Kanali Petro Ngata, ametoa maagizo hayo leo tarehe 12 Augosti 2022, alipokuwa katika ziara ya kukagua shamba hilo lililopo katika kijiji cha Bassotu , Wilaya ya Hanang'i Mkoani Manyara.
Kanali Ngata ameongeza kuwa Bassotu kuna faida kubwa endapo SUMAJKT itafanikiwa kupata eneo kubwa na kuanza na aina ya mazao mawili ambayo ni ngano na katamu (alizeti za miba).
"Ngano na katamu ni mazao ambayo tukizalisha tutakuwa na uhakika wa kupata faida" ameeleza Kanali Ngata.
Aidha, Kanali Petro Ngata, ameeleza kuwa shirika litaanza kuliwekea mipango mizuri na ya haraka shamba hilo, endapo msajili wa hazina atakubali kutoa eneo kwa SUMAJKT.
Kwa upande wa Meneja wa mradi wa shamba la kilimo cha alizeti SUMAJKT Bassotu Sajinitaji Bahati Kidenya, amesema kuwa mradi huo ulianzishwa mwaka 2017 kwa ajili ya kuongeza mapato ya shirika na uchumi wa Taifa.
Sajinitaji Kidenya, ameongeza kuwa mradi wa shamba la SUMAJKT Bassotu , uliopo wilayani Hanang'i una jumla ya hekari 1000 kati ya hizo zinazofaa kwa kilimo kwa sasa ni hekari 500.
Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata, katika ziara hiyo pia alipitia katika Halmashauri ya mji wa Hanang'i, ambapo alipokelewa na Katibu Tawala (DAS) Hanang'i Mhe. Paul Bura, ambapo ameeleza kuwa uwepo wa SUMAJKT katika kijiji cha Bassotu kumepunguza matukio ya uhalifu kwa kiasi kikubwa.
Mhe. Bura Ameongeza kuwa SUMAJKT na uongozi wa wilaya hiyo hapo awali kulikuwepo na makubaliano ya uanzishwaji wa kituo cha zana za kilimo pamoja na ujenzi wa kiwanda cha mafuta ya alizeti kwa sababu malighafi zinapatikana za kutosha.
SUMAJKT imekuwa ikijihusisha na uwekezaji wa aina mbali mbali ikiwemo kilimo.
ok
ReplyDelete