Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Tanzania Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele apongezwa na Mkuu wa JKT Zambia kwa kupiga hatua katika kusimamia uzalishajimali .
Kamanda wa Jeshi la Kujenga Taifa Zambia Luteni Jenerali Maliti Solochi tarehe 15 Machi 2022 ametembelea Kiwanda cha maji SUMAJKT Bottling Company pamoja na kiwanda cha ushonaji nguo SUMAJKT Garments Company katika eneo la Mgulani JKT Dar es Salaam kuona uzalishajimali na ametoa pongezi kwa namna Shirika linavyoendeshwa na kupiga hatua chini ya Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajab Nduku Mabele.
Jenerali Solochi amesema kuwa JKT Zambia limekopi kila kitu kutoka JKT Tanzania ikiwemo uanzishaji wa viwanda na kwasasa jeshi lao lina baadhi ya viwanda ikiwemo kiwanda cha maji na kiwanda cha viatu.
Jenerali Solochi ameongeza kuwa mahusiano haya ya kindugu kati ya JKT Tanzania na JKT Zambia yalianzishwa na Viongozi waasisi wake ambao ni baba wa taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Keneth Kaunda ambao ndio chanzo cha kuanzishwa kwa vyombo hivyo .
Comments
Post a Comment