Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Kanali Petro Ngata ameendelea na ziara katika miradi mbali mbali ya ujenzi inayoendelea kujengwa na Kampuni ya ujenzi “SUMAJKT Construction Company Limited kupitia SUMAJKT Ujenzi kanda ya ziwa.
Kanali Petro Ngata katika ziara hiyo iliyoanza tarehe 28 hadi 30 Oktoba 2022 amekagua miradi mingine
inayotekelezwa na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa ambayo ni mradi wa Ujenzi wa hanga la Askari, Jengo la kuhifadhia maiti "Mortuary" na Jengo la wodi ya Wagonjwa Maalumu "VIP Ward" katika Hospitali ya Kijeshi Ilemela- Mwanza,
ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Kanda ya Ziwa lililopo Busweli-Ilemela Jijini Mwanza na kuagiza SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Ziwa iongeze kasi ya ujenzi ili ikamilishe mradi huo kwa wakati.
Aidha Kanali Petro Ngata amepongeza maendeleo ya utekelezaji wa Miradi hiyo na kuagiza SUMAJKT Ujenzi Kanda ya ziwa kukamilisha Ujenzi wa hanga la Askari pamoja na chumba cha kuhifadhia maiti ndani ya wiki mbili kuanzia tarehe 30 Oct 22 na pia kukamilisha Ujenzi wa "VIP Ward" ifikapo mwishoni mwa mwezi Dec 22.
SUMAJKT imekuwa ikitekeleza miradi mbali mbali ya ujenzi kote nchini kupitia kampuni yake ya ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited ambayo nayo imekuwa ikitekeleza miradi hiyo kupitia kanda ya karibu na eneo la mradi husika.
SUMAJKT Construction Company Limited ina kanda saba za ujenzi ambazo ni SUMAJKT Ujenzi Makao Makuu, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Kati, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Mashariki, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Magharibi, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Kaskazini, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Nyanda za juu Kusini na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya ziwa.
Comments
Post a Comment