Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan amempongeza Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa kukamilisha ujenzi wa Mradi wa Chuo cha Ualimu Kabanga .
Mhe. Rais Samia Suluhu amesema hayo tarehe 17 Oktoba 2022 katika ufunguzi wa majengo ya chuo hicho kilichopo katika wilaya ya Kasulu, Mkoa wa Kigoma alipokuwa akizindua Mradi huo
Aidha mradi huo uliofadhiliwa na Serikali ya Canada Ulianza tarehe 26 Machi 2019 ambapo ulitekelezwa na Kampuni ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited na kukabidhiwa rasmi kwa Wizara ya Elimu baada ya kukamilika tarehe 21 Apri 2022 kupitia Kanda ya ujenzi ya Kusini inayosimamiwa na Kanali Mbaraka Magogo ambaye ni Mkuu wa Ujenzi Kanda ya Magharibi.
Thamani ya mradi huo ni TShs 12.1 billion zikiwa ni gharama za mkandarasi na una jumla ya majengo 13 ambayo ni mabweni 2, jengo la utawala, jengo la madarasa lenye madarasa 10, Bwalo, Ukumbi wa mikutano , jengo la maabara, ukumbi wa mihadhara, jengo la maktaba, zahanati na nyumba 4 za watumishi na yote yakiwa ndani ya Uzio.
Pia mradi huo una miundombinu ya Biogas, Tehama, Umeme na Maji.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele ametoa kompyuta mbili kama mchango kwenye maabara ya chuo hicho ambazo amezikabidhi kwa Katibu Mkuu Elimu siku ya uzinduzi.
Mradi huo upo katika Kipindi cha uangalizi cha mwaka mmoja kuanzia tarehe 21 Aprili 2022 ambacho kitakamilika tarehe 20 Aprili 2023.
Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa Limekuwa likikamilisha ujenzi wa miradi mbali mbali kupitia Kampuni yake ya Ujenzi SUMAJKT Construction Company Limited yenye kanda saba za ujenzi ambazo ni SUMAJKT Ujenzi Makao Makuu, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Kati, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Mashariki, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Magharibi, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Kaskazini, SUMAJKT Ujenzi Kanda ya Nyanda za juu Kusini na SUMAJKT Ujenzi Kanda ya ziwa.
Comments
Post a Comment